Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian Leo Julai 20, 2023 amepokea Kombe la NBC PREAMIER LEAGUE ambalo litakwenda kutumika msimu wa 2023/2024.
Akipokea kombe hilo, Mkuu wa Mkoa ametoa wito kwa wanatabora kuiunga mkono timu ya Tabora United ambayo inakwenda kushiriki kwenye Ligi Kuu mwaka huu.
“Mimi niwaambie tu wanatabora tuendelee kushirikiana na kutoa hamasa tuliokuwa nayo toka awali na tujitokeze pale inapohitajika ili tuipe nguvu timu yetu”
Sambamba na hilo ameipongeza Benki ya NBC ambayo ndio mdhamini mkuu kwa kujitoa na kushiriki kwao kwenye shughuli za kijamii.
“tunawapongeza kwa Kazi nzuri mnayofanya kwani mmekuwa na mchango mkubwa sana kwa jamii”
Itakumbukwa kuwa, Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa Michezo mnamo Mei 12, 2023 walifanikiwa kuipandisha daraja timu ya KITAYOSCE (Tabora United) na kufanikiwa kufuzu kwenye Ligi Kuu ya NBC msimu wa 2023/2024.
Tabora
S.L.P: 25 Tabora
Simu: 026 2604058
Mobile:
Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz
Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa