Picha zikionesha Uzinduzi wa Mradi wa ujenzi wa barabara ya lami Usoke-Center 1 yenye urefu wa Kilomita 1.5 iliyopo Usoke Wilayani Urambo. Imesimamiwa na TARURA ambapo jumla ya shilingi milioni 750 zimetumika kukamilisha mradi huo ambao umekamilika kwa asimia 100 na tayari umeshanza kutumika na Wananchi wa Usoke.
Mradi huu wa ujenzi wa barabara ya lami Usoke-Center 1 ni miongoni mwa miradi nane (8) ambayo imepitiwa na kuzinduliwa na Mwenge wa Uhuru katika Halmashauri ya Wilaya ya Urambo. Ambapo Mapema leo Mkuu wa Wilaya ya Urambo Mhe. Kenani Kihongosi aliupokea kutoka Wilaya ya Kaliua
Mwenge wa Uhuru uliwasili Mkoani Tabora Septemba 14, 2023 na kupokelewa na Mkuu wa Mkoa Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian katika Viwanja vya Shule ya Sekondari Kiloli, Wilayani Sikonge. ambapo utahitimisha mbio zake ukiwa umezindua jumla ya miradi 50 yenye thamani ya Shilingi Bilioni 22.2 na kukabidhiwa Mkoa wa Singida Septemba, 21, 2023.
Kauli Mbiu ni "Tunza Mazingira, Okoa Vyanzo vya maji kwa ustawi wa Viumbe Hai na Uchumi wa Taifa.
Tabora
S.L.P: 25 Tabora
Simu: 026 2604058
Mobile:
Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz
Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa