Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Elimu), Dkt. Charles Msonde ameziagiza halmashauri za Wilaya ya Urambo na Kaliua Mkoani Tabora kuongeza nguvu kazi ya Mafundi na usimamizi kwa kufanya kazi usiku na mchana katika ujenzi wa miundombinu yote ya shule mpya, Vyumba vya Madarasa, Mabweni na Vyoo vinyoendoendelea kujengwa ili viweke kukamilika kwa wakati.
Ameelekeza hayo tarehe 24 Juni 2023 wakati akikagua ujenzi wa miundombinu ya ujenzi wa Shule Mpya na Madarasa, Mabweni na vyoo katika shule za Msingi na kidato cha sita katika wilaya za Urambo na Kaliua vinavyoendelea kujengwa kupita miradi ya BOOST na BARRICK.
Dkt. Msonde amewaagiza Wakurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya za Urambo na Kaliua kuhakikisha wanaongeza usimamizi katika ujenzi wa miundombinu hiyo ijengwe usiku na mchana kuhakikisha ifikapo tarehe 30 Juni 2023 miundombinu yote kupitia mradi wa BOOST iwe imekamilika.
Kadhalika, Dkt. Msonde amempongeza Mkurungenzi wa halmashauri ya Kaliua kwa kasi nzuri ya ujenzi shule za isingi mpya za Magele na Mange ambazo zipo katika hatua nzuri ujenzi.
Dkt. Msonde amefafanua kuwa mwezi Aprili 2023, Serikali ilitoa fedha kwa ajili ya ujenzi na ukarabati wa miundombinu ya shule za msingi kupitia mradi wa BOOST ambapo Mkoa wa Tabora umepata jumla ya shilingi Bilioni 12.1 kwa ajili ya ujenzi wa shule za msingi mpya 17, vyumba vya madarasa 118, vyumba vya madarasa ya mfano ya Elimu ya Awali 16, matundu ya vyoo 130 na nyumba za walimu 2 (2 in 1, ambapo miundombinu hiyo inapaswa kukamilika ifikapo tarehe 30 Juni 2023.
Tabora
S.L.P: 25 Tabora
Simu: 026 2604058
Mobile:
Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz
Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa