Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mh. Balozi Dkt Batilda S. Buriani afungua kikao cha tathmini ya utekelezaji wa viashiria vya mkataba wa lishe ngazi ya mkoa. katika ufunguzi huo, Mkuu wa Mkoa amezipongeza Halmashauri zote za Mkoa wa Tabora kwa kutekeleza maelekezo ya Serikali ya kutenga Tsh 10,000/= kwa kila mtoto chini ya miaka mitano katika mipango na bajeti ya 2022/2023.
Aidha ametoa maelekezo kwa Wakurugenzi na Waweka hazina wa Halmashauri kuhakikisha fedha zote zilizotengwa kutekeleza Afua za lishe ziweze kutolewa na kutekeleza Afua hizo kama ilivyo kusudiwa.
Mkuu wa Mkoa amewataka Waganga wakuu wa Halmashauri kuhakikisha vidonge vya kuongeza wekundu wa damu wa akina mama wajawazito havikosekani kwenye vituo vya kutolea huduma za afya ili akina mama hawa wasikose huduma hii wafikapo katika vituo vya kutolea huduma za afya.
Aidha, mkuu wa Mkoa, ametoa maelekezo kwa Waheshimiwa wakuu wa Wilaya kuhakikisha wanahamasisha jamii kipindi hiki cha kampeni ya mwezi wa afya na lishe ya mtoto iliyoanza tarehe 18//2022 hadi tarehe 18/8/2022 ili waweze kupeleka watoto wote wenye umri wa miezi 6-59 katika vituo vya kutolea huduma za afya waweze kupata nyongeza ya matone ya Vitamin A kwa ajili ya kuimarisha kinga za miili yao , ukuaji mzuri wa mwili na akili zao.
Tabora
S.L.P: 25 Tabora
Simu: 026 2604058
Mobile:
Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz
Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa