Wakazi wa halmashauri ya Manispaa ya Tabora wameishukuru Serikali kupitia wakala wa barabara za mijini na vijijini TARURA kuanza ujenzi wa barabara ya kiwango cha Lami Manipaa ya Tabora yenye urefu wa mita 1800, wenye thamani ya Shilingi Milioni 913.8, Fedha ambazo zilizotokana mfuko wa jimbo kiasi cha shilingi Milioni 492.3 na kiasi cha shilingi milioni 421.8 makusanyo ya tozo za mafuta (Fuel Levy). Mradi huu unatarajiwa kukamilika mwaka 2024..
Barabara hiyo ambayo ujenzi wake unagharimu kiasi cha shilingi Milioni 913.8 imewekewa jiwe la msingi leo Septemba 15, 2023 na kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2023 Abdallah Shaib Kaim.
Wakazi wa kata ya Mpera wamesema barabara hiyo pindi itakapokamilika itawasaidia kurahisha shughuli mbalimbali za uchumi ikiwemo usafirishaji na pia itapunguza changamoto ya usafiri kipindi cha masika.
Nae,Mkimbiza mwenge Kitaifa 2023 Ndugu,Adallah Shaib Kaim amewahimiza wasimamizi wa mradi ambao ni TARURA kumsimamia vyema mkandarasi kutoka kampuni ya ujenzi ya SAMOTA ili aweze kukamilisha barabara hiyo kwa wakati ulipangwa kwenye mkataba.
Mradi huu wa Ujenzi wa Barabara ya Lami ni miongoni mwa miradi sita (6) ambayo imepitiwa na kuzinduliwa na Mwenge wa Uhuru katika Halmashauri ya Wilaya ya Tabora. Ambapo Mapema leo Mkuu wa Wilaya ya Tabora Mhe. Peter Bura aliupokea kutoka Wilaya ya Sikonge.
Tabora
S.L.P: 25 Tabora
Simu: 026 2604058
Mobile:
Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz
Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa