Wakazi wa Kijiji cha Nhandwe Wilayani Kaliua wameishukuru Serikali kupitia Wakala wa Barabara za Mijini na Vijijini TARURA kwa kusimamia na kukamilisha ujenzi wa daraja la Ichemba- Nhwande uliogharimu zaidi ya shilingi Milioni mia tisa, fedha kutoka Serikali Kuu, ambao umekamilika na umeshaanza kutumika.
Daraja hilo lenye urefu wa mita mita 30, na Upana mita 11 limezinduliwa leo Septemba 16, 2023 na kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2023 Abdallah Shaib Kaim.
Wakazi wa Kijiji cha Nhwande wamesema, kukamilika kwa ujenzi wa daraja hilo kumesaidia sana kupunguza changamoto ya usafiri hasa nyakati za mvua na kwamba hapo awali wananchi walikuwa wakipata shida kufika baadhi ya maeneo muhimu kwa ajili ya kupata huduma mbalimbali zikiwemo za afya. Na kumeripotiwa vifo kadhaa vya mama wajawazito kutokana na kukosa huduma. Na hivyo wamezidi kutoa shukrani kwa Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutoa fedha nyingi na kuhaidi kuirinda miundombinu ya daraja hilo.
Nae,Mkimbiza Mwenge Kitaifa 2023 Ndugu,Adallah Shaib Kaim ameupongeza Uongozi wote wa Wilaya ya Kaliua kwa kusimamia mradi huu ambao Serikali imetoa fedha nyingi, na kuwataka Wananchi wa Nhwande kuumtambua mchango mkubwa wa Serikali katika maendeleo ya wananchi.
Mradi huu wa Ujenzi wa Daraja la Ichemba- Nhwande ni miongoni mwa miradi sita (6) ambayo itapitiwa na kuzinduliwa na Mwenge wa Uhuru katika Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua. Ambapo Mapema leo Mkuu wa Wilaya ya Kaliua Mhe. Dkt. Chuachua aliupokea kutoka Wilaya ya Tabora
Mwenge wa Uhuru uliwasili Mkoani Tabora Septemba 14, 2023 na kupokelewa na Mkuu wa Mkoa Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian katika Viwanja vya Shule ya Sekondari Kiloli, Wilayani Sikonge ambapo utahitimisha mbio zake ukiwa umezindua jumla ya miradi 50 yenye thamani ya Shilingi Bilioni 22.2, katika Halmashauri zote nane (8) na kukabidhiwa Mkoa wa Singida Septemba, 21, 2023.
Kauli Mbiu ni "Tunza Mazingira, Okoa Vyanzo vya maji kwa ustawi wa Viumbe Hai na Uchumi wa Taifa.
Tabora
S.L.P: 25 Tabora
Simu: 026 2604058
Mobile:
Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz
Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa