Kiongozi wa mbio za Mwenge Kitaifa Ndugu, Abdallah Shaib, leo Septemba 15, 2023 amezindua mradi wa Ufyatuaji wa matofali wa Kikundi cha Vijana cha Britght Vision chenye wanachama kumi (10) kilichopo Manispaa ya Tabora, ambao umegharimu fedha za kitanzania shilingi milioni 27.6, ambao pia umekamilika kwa asilimia mia na tayari shughuri za uzalishaji zimeshaanza.
Wakitoa taarifa kwa kiongozi wa Mbio za Mwenge kifaita, wameeleza kuwa kukamilika kwa mradi huo ni mkopo wa milioni 20 kutoka Halmashauri ma shilingi milioni 7.6 ni michango ya wanachama na harambee kutoka kwa wadau mbalimbali wa maendeleo. Na hivyo wametoa shukrani kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuhakikisha vijana wanafaidika na mikopo inayoendelea kutolewa na Halmashauri zetu.
Akiongea na hadhara ya wananchi Wilayani Tabora, Ndugu Abdalah Shaibu Kaim ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Tabora pamoja na wadau mbalimbali wa maendeleo kwa kuhakikisha vijana hao wanapata fedha na kuanzisha mradi huo ambao una tija kwa vijana hao na wananchi kwa ujumla. Serikali inaendelea kutenga fedha kupitia halamashauri zeti kwa lengo la kuwasaidia vijana.
Mradi huu wa vijana ni miongoni mwa miradi sita (6) ambayo imepitiwa na kuzinduliwa na Mwenge wa Uhuru katika Halmashauri ya Wilaya ya Tabora. Ambapo Mapema leo Mkuu wa Wilaya ya Tabora Mhe. Peter Bura aliupokea kutoka Wilaya ya Sikonge.
Tabora
S.L.P: 25 Tabora
Simu: 026 2604058
Mobile:
Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz
Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa