Mkimbiza Mwenge Kitaifa 2023 Ndugu, Adallah Shaib Kaim leo Septemba 17, 2023 amezindua mradi wa Ujenzi wa Shule ya Awali na Msingi Samia iliyopo Kata ya Urambo, Wilayani Urambo, ujenzi huo umegharimu kiasi cha shilingi milioni 562. ambapo kiasi cha shilingi milioni 561.1 zilitoka kwa Wahisani na Shilingi Milioni 1.5 michango ya wananchi na jumla ya wanafunzi 900 kufaidika na mradi huu.
Akisoma taarifa ya mradi, Mwl. Grace Ishengoma amesema “awali wanafunzi walikuwa wakisongamana, hali iliyosababisha watoto wengi kuacha kwenda shule. Na hivyo uwepo wa shule hii kutasaidia kutoa nafasi kwa watoto kupata elimu kwa urahisi. Na mwisho alimshukuru Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutoa fedha nyingi kwenye sekta ya elimu.
Mradi huu wa Ujenzi wa Shule ya Msingi Samia ni miongoni mwa miradi nane (8) ambayo itapitiwa na kuzinduliwa na Mwenge wa Uhuru katika Halmashauri ya Wilaya ya Urambo. Ambapo Mapema leo Mkuu wa Wilaya ya Urambo Mhe. Kenani Kihongosi aliupokea kutoka Wilaya ya Kaliua
Mwenge wa Uhuru uliwasili Mkoani Tabora Septemba 14, 2023 na kupokelewa na Mkuu wa Mkoa Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian katika Viwanja vya Shule ya Sekondari Kiloli, Wilayani Sikonge. ambapo utahitimisha mbio zake ukiwa umezindua jumla ya miradi 50 yenye thamani ya Shilingi Bilioni 22.2 na kukabidhiwa Mkoa wa Singida Septemba, 22, 2023.
Kauli Mbiu ni "Tunza Mazingira, Okoa Vyanzo vya maji kwa ustawi wa Viumbe Hai na Uchumi wa Taifa.
Tabora
S.L.P: 25 Tabora
Simu: 026 2604058
Mobile:
Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz
Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa