Picha zikionesha Kiongozi wa Mbio za Mwenge kitaifa Ndugu Abdalla Shaib akitembelea na kukagua Kikundi cha Vijana cha BODABODA - KAZI IENDELEE kilichopo Ugowola Wilayani Uyui. Ambapo kikundi hiko kilipatiwa jumla ya shilingi milioni 10 kama sehemu ya mkopo wa asilimia 4 ya mapato ya ndani ya Halmashauri kupitia Ustawi wa Jamii na kufanikiwa kuanzisha mradi wa Usafirishaji wa abiria kwa pikipiki (Bodaboda).
Mradi huu wa vijana ni miongoni mwa miradi saba (7) ambayo itapitiwa na kuzinduliwa na Mwenge wa Uhuru katika Halmashauri ya Wilaya ya Uyui. Ambapo Mapema leo Mkuu wa Wilaya ya Uyui Mhe. Zakaria Mwansasu aliupokea kutoka Wilaya ya Urambo.
Mwenge wa Uhuru uliwasili Mkoani Tabora Septemba 14, 2023 na kupokelewa na Mkuu wa Mkoa Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian katika Viwanja vya Shule ya Sekondari Kiloli, Wilayani Sikonge. ambapo utahitimisha mbio zake ukiwa umezindua jumla ya miradi 50 yenye thamani ya Shilingi Bilioni 22.2 na kukabidhiwa Mkoa wa Singida Septemba, 22, 2023.
Kauli Mbiu ni "Tunza Mazingira, Okoa Vyanzo vya maji kwa ustawi wa Viumbe Hai na Uchumi wa Taifa.
Tabora
S.L.P: 25 Tabora
Simu: 026 2604058
Mobile:
Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz
Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa