Mwenge wa Uhuru wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, leo Septemba 18, 2023 umepokelewa Wilayani Uyui, ukitokea Wilaya ya Urambo.
Mkuu wa Wilaya ya Uyui Mhe. Zakaria Mwansasu ameupokea Mwenge huo na kukimbizwa umbali wa kilomita 263.6 kukagua, kuona, kuzindua na kuweka mawe ya msingi miradi Saba (7) ikiwemo ya Elimu, Afya, Maji na Umeme na maendeleo ya jamii yenye thamani ya Shilingi Bilioni 4.4
Mwenge wa Uhuru uliwasili Mkoani Tabora Septemba 14, 2023 na kupokelewa na Mkuu wa Mkoa Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Buria Viwanja vya Shule ya Sekondari Kiloli, Wilayani Sikonge, na kuhitimisha mbio zake na kukabidhiwa Mkoa wa Singida Septemba, 22. 2023, ukiwa umezindua jumla ya miradi 50 yenye thamani ya Shilingi Bilioni 22.2, katika Halmashauri zote nane (8) za Tabora.
Kauli Mbiu ni "Tunza Mazingira, Okoa Vyanzo vya maji kwa ustawi wa Viumbe Hai na Uchumi wa Taifa.
Tabora
S.L.P: 25 Tabora
Simu: 026 2604058
Mobile:
Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz
Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa