• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Nukushi ya malalamiko |
TABORA REGION ADMINISTRATIVE SECRETARY

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi Ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tabora

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Biashara
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo Cha Mawasiliano
    • Muundo
  • Wilaya
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Wilaya ya Urambo
    • Wilaya ya Igunga
    • Wilaya ya Uyui
    • Wilaya ya Kaliua
    • Wilaya ya Sikonge
    • Wilaya ya Nzega
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Tabora
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Halmashauri ya Wilaya ya Igunga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua
    • Halmashauri ya Wilaya Urambo
    • Halmashauri ya Mji wa Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya Sikonge
  • Fursa za Uwekezaji
    • Miombo Project
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi inayoendelea
    • Kilimo
      • Miombo Project
        • Miradi iliyokamilika
        • Miradi inayoendelea
    • Mifugo
    • Opportunity services
    • Viwanda na Biashara
      • New menu item
    • Madini
    • Uvuvi
    • EQUIP-TANZANIA
    • FURSA ZA UWEKEZAJI
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Tafiti
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

MWENYEKITI WA CCM MKOA WA TABORA AFUNGUA KONGAMANO LA MAADHIMISHO YA MIAKA 48 YA CHAMA CHA MAPINDUZI.

Posted on: February 3rd, 2025

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Tabora, Ndg. Said Juma Nkumba, amefungua kongamano la kilele cha maadhimisho ya miaka 48 ya kuzaliwa kwa chama hicho, lililofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tabora.

Akizungumza katika hafla hiyo, Ndg. Nkumba ameupongeza umoja wa wazee mashuhuri wa historia na ushauri wa Tabora kwa kuandaa kongamano hilo kwa kushirikiana na uongozi wa CCM Mkoa wa Tabora na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tabora. Amesema mkoa wa Tabora umechukua nafasi muhimu katika historia ya harakati za kudai uhuru wa nchi yetu, huku akiwapongeza wataalam wa mkoa kwa juhudi zao katika kusimamia miradi ya maendeleo kwa ustadi mkubwa.

"Watumishi wetu wa serikali wanafanya kazi kubwa ya kusimamia fedha na rasilimali, ambazo kwa kweli zinatumika vyema na jamii inazidi kunufaika," alisema Ndg. Nkumba. "Endeleeni kufanya hivyo na sisi kazi yetu kubwa ni kuendelea kuwatia moyo ili muweze kuendelea kutekeleza majukumu yenu."

Katika kongamano hilo, Mzee Mohamed Said Salum, Mwandishi wa Vitabu na Mtaalamu wa Historia, alitoa mada kuhusu mchango wa mkoa wa Tabora katika historia ya ukombozi wa Tanganyika. Amesisitiza kuwa mkoa wa Tabora ni chimbuko la harakati za kudai uhuru na amewataka wananchi kupuuza propaganda za historia zilizopotoshwa, hasa kuhusu biashara ya watumwa. Amesema ni muhimu kujikita katika kuandika na kuhifadhi historia ya mashujaa wa hivi karibuni waliopigania uhuru.

Kwa upande wake, Katibu Tawala wa Mkoa wa Tabora, akimwakilisha Mkuu wa Mkoa, Dkt. John Rogath Mboya, amesema uchumi na maendeleo ya mkoa wa Tabora yanaendelea vizuri. Amebainisha kuwa pato la mkoa limeongezeka na kufikia shilingi trilioni 5.476, na wastani wa pato la mtu mmoja katika mkoa huo ni shilingi 1,850,000 kwa takwimu za mwaka 2024.

Dkt. Mboya ameongeza kuwa zaidi ya shilingi trilioni 1.1 zimepokelewa katika sekta mbalimbali ikiwemo elimu, afya, kilimo, mifugo, nishati, miundombinu na uwekezaji, na kuahidi kuwa serikali itaendelea kushughulikia masuala ya maendeleo kwa umakini mkubwa.

Alimaliza kwa kutoa wito kwa viongozi wa dini na wananchi wa mkoa wa Tabora kuwa mstari wa mbele katika kusimamia maadili mema na kupinga mambo yasiyofaa katika jamii, akisema kuwa serikali itaendelea kutekeleza wajibu wake kwa kuhakikisha maadili yanaenziwa katika jamii.

Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 18, 2023
  • SIKU YA KIMATAIFA YA WANAWAKE MACHI 8 March 07, 2024
  • BEI ELEKEZI YA MBOLEA YA CAN KWA KAMPUNI YA YARA June 15, 2022
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MITAALA YA ELIMU TANZANIA BARA March 23, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • BARAZA LA BIASHARA MKOA WA TABORA LADHAMIRIA KULETA MAGEUZI KATIKA KUBORESHA MAZINGIRA YA BIASHARA NA UWEKEZAJI KWA WANANCHI

    May 21, 2025
  • VIONGOZI WA MIKOA YA TABORA NA KIGOMA WAFANYA KIKAO CHA MAANDALIZI KUELEKEA MAONESHO YA SIKUKUU YA WAKULIMA NANE NANE 2025

    May 20, 2025
  • RC CHACHA AZINDUA MASHINDANO YA UMITASHUMTA NA UMISSETA MKOA WA TABORA, ATOA WITO WA KULINDA NDOTO ZA WATOTO.

    May 19, 2025
  • TABORA YAADHIMISHA SIKU YA KIMATAIFA YA FAMILIA KWA KUTOA WITO WA MALEZI BORA NA KUPINGA UKATILI.

    May 15, 2025
  • Angalia zote

Video

VIJANA WAKAA MEZA MOJA NA RC MKOA WA TABORA
video nyingine

Viungio vya Haraka

  • Maelezo na fomu ya ahadi ya uadilifu kwa watumishi wa umma
  • Guidelines for the use of ICT in government
  • Agriculture
  • MALALAMIKO,PONGEZI NA MAONI INGIA HAPA
  • Bofya hapa Eoffice

Tovuti Muhimu

  • Ikulu
  • Ofisi ya Rais-Tamisemi
  • Ofisi ya Rais-Utumishi
  • SALARYSLIP
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tabora

    S.L.P: 25 Tabora

    Simu: 026 2604058

    Mobile:

    Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa mara
    • Service
    • owner

Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa