Kupitia kikao cha kamati ya ushauri ya mkoa wa Tabora (RCC), Sekretarieti ya Mkoa wa Tabora imewaomba wajumbe wa kikao hiko kupitisha bajeti shilingi bilioni 387.4 kwa ajili ya kutekeleza miradi na shughuri mbalimbali za mkoa wa Tabora kupitia bajeti ya mwaka 2024/2025. Hayo yamejiri leo katika kikao cha kamati ya ushauri ya mkoa kinachoendelea kufanyika katika ukumbi wa Isike Mwanakiyungi, Machi 16, 2024
Akisoma taarifa kwa niaba ya Katibu Tawala Msaidi Mipango na Uratibu Bwan. Fedrick Ichwekeleza amesema kwa mwaka wa fedha wa 2024/2025 mkoa wa Tabora unataraji kutekeleza miradi ya maendeleo na shughuri mbalimba za uendeshaji kupitia makisio ya bajeti ya shilingi Bilioni 387.4 ikiwa ni moja ya utekelezaji wa takwa la kisheria ya bajeti Na. 11 ya mwaka 2015.
Aidha. Bwan. Fredick amebainisha vipamumbele vya mkoa vikiwemo kukuza uwekezaji, kuhimarisha huduma za elimu na afya, kutoa mikopo yenye unafuu, kuhimarisha upatikanaji wa maji, sambamba na kukuza utendaji wa kazi katika ofisi ya mkuu wa Mkoa wa Tabora, na hivyo kupitishwa ka bajeti hiyo kutasaidia kukamilisha vipaumbele hivyo.
Ikumbukwe kuwa, kikao hiki cha kamati ya ushauri ya Mkoa wa Tabora hufanyika mara mbili kila mwaka ambapo kikao cha kwanza kimefanyika leo Machi 16, 2024 na kikao cha pili kinatarajiwa kufanyika mwezi Disemba mwaka huu.
Tabora
S.L.P: 25 Tabora
Simu: 026 2604058
Mobile:
Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz
Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa