Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian amekutana na kufanya mazungumzo na uongozi wa Taasisi ya Boma Foundation iliyo na makao makuu yake Mkoani Dar Es Salaam kwa lengo la kujadiliana miradi mbalimbali ya kimaendeleo mkoani Tabora.
Mhe. Mkuu wa Mkoa ameushukuru uongozi mzima wa Boma Foundation kwa kuchagua mkoa wa Tabora kuwa miongoni mwa mikoa ambayo itafaidika na uwekezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo itakayoanzishwa na taasisi hiyo.
Na kuongeza kuwa, Mkoa wa Tabora kwa kushirikiana na wataalamu waliopo katika halmashauri zote, watahakikisha wanaweka mazingira mazuri na wezeshi kwa miradi yote itakayoanzishwa na taasisi hiyo.
Aidha Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa amebainisha fursa za uwekezaji zilizopo mkoani Tabora zikiwemo, hususani kilimo cha pamba, ufugaji wa nyuki na uwekezaji upande malazi hasa ujenzi wa hotel za kisasa.
Naye Ndugu. Omari Issa Mwenyekiti wa Boma Foundation amemshukuru Mkuu wa Mkoa wa Tabora kwa kuweka mazingira mazuri kwa taasisi zenye uhitaji wa kuwekeza mkoani humo kwani mkoa wa Tabora umebarikiwa kuwa na fursa nyingi kwa kuzingatia jiografia ya mkoa huo. Na kumuahidi Mkuu wa mkoa kutumia watalaamu waliopo kwenye taasisi hiyo kwa kutumia uzoefu na ujuzi walionao kuanzisha miradi ya maendeleo.
Kwa niaba ya wataalamu Mkoa wa Tabora, Mkurugenzi wa Manispaa ya Tabora Ndugu. Elias Kayandabila amehaidi kutoa ushirikiano kwa taasisi ya Boma Foundation kwa kuweka mazingira wezeshi kwa kushirikiana na wataalamu waliopo kwenye halmashauri ili kuhakikisha miradi hiyo inakuwa na tija kwa wananchi wa mkoa wa Tabora.
Tabora
S.L.P: 25 Tabora
Simu: 026 2604058
Mobile:
Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz
Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa