Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian ameshiriki zoezi la usafi lililofanyika katika Stendi Mpya ya Mabasi yaendayo mikoani iliyopo Manispaa ya Tabora, Januari 23, 2024, na kuhudhuriwa na mamia ya wananchi na watendaji mbalimbali kutoka, Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Tabora, Manispaa ya Tabora na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tabora.
Akiongea na wananchi waliojitokeza, Mhe Mkuu wa Mkoa ametoa wito kwa wananchi wa Mkoa wa Tabora kuzingatia suala la usafi wa Mazingira ili kukabiliana na magonjwa ya milipuko. Na kuutaka uongozi wa Stendi ya Mabasi ya Mkoa wa Tabora kwa kushirikia na Halmashauri kuhakikisha wanaunda sheria itakayosimamia masuala ya usafi.
Sambamba na hilo Mhe. Batilda Burian amewapongeza baadhi ya wananchi waliojitokeza kushiriki katika zoezi hilo la usafi ambalo kwa siku ya leo limefanyika nchi nzima, na kuendelea kulienzi neno “unyamwezini” lenye maana ya usafi/ustaarabu sambamba na kujenga utamaduni wa kuwa “viherehere” hasa kwenye mambo yenye tija kwenye jamii.
Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Manispaa ya Tabora Ndugu. Elias Kayandabila amemshukuru Mkuu wa Mkoa wa Tabora kwa kushiriki zoezi la usafi na kumuahidi kuyafanyia kazi maelekezo yote yliotolewa.
Tabora
S.L.P: 25 Tabora
Simu: 026 2604058
Mobile:
Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz
Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa