Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian akitoa taarifa ya Mkoa kuhusiana na maendeleo ya Sekta ya Afya kwa Kamati ya Bunge ya Afya na UKIMWI iliyofika Mkoani Tabora kwa ziara ya kikazi ya siku mbili.
Katika taarifa yake, Mhe. Mkuu wa Mkoa ameleezea mafanikio makubwa katika sekta ya Afya ambayo yamefanyika kwa kipindi cha miaka miwili ya uongozi wa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Uboreshwa huo unagusia mambo kama ujenzi wa Majengo ya wagonjwa wa dharula (EDM) na wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalumu(ICU), ujenzi wa hospitali za Wilaya na vituo vya afya na kupungua kwa vifo vya mama wajawazito.
Sambamba na hilo Mhe. Dkt. Batilda ameelezea baadhi ya changamoto ambazo zinaukabili Mkoa zikiwemo, ongezeko la madimbwi na mazalia ya mbu, Mkoa kutoingizwa kwenye mpango wa taifa wa kupulizia dawa na imani potofu.
Aidha Mhe.Mkuu wa Mkoa ameeleza jitihada za Mkoa kukabiliana na changamoto zinazoikabili sekta ya afya, ikiwemo kushirikisha wadau mbalimbali, kutoa elimu kupitia vyombo vya habari vilivyopo, Halmashauri kutenga fedha za usafi, ugawaji wa vyandarua na utolewaji wa semina kwa watumishi wa Afya.
Kamati ya Bunge ya Afya na UKIMWI itakuwa na ziara ya siku mbili (2) katika Wilaya ya Tabora na Uyui.
Tabora
S.L.P: 25 Tabora
Simu: 026 2604058
Mobile:
Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz
Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa