• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Nukushi ya malalamiko |
TABORA REGION ADMINISTRATIVE SECRETARY

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi Ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tabora

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Biashara
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo Cha Mawasiliano
    • Muundo
  • Wilaya
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Wilaya ya Urambo
    • Wilaya ya Igunga
    • Wilaya ya Uyui
    • Wilaya ya Kaliua
    • Wilaya ya Sikonge
    • Wilaya ya Nzega
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Tabora
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Halmashauri ya Wilaya ya Igunga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua
    • Halmashauri ya Wilaya Urambo
    • Halmashauri ya Mji wa Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya Sikonge
  • Fursa za Uwekezaji
    • Miombo Project
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi inayoendelea
    • Kilimo
      • Miombo Project
        • Miradi iliyokamilika
        • Miradi inayoendelea
    • Mifugo
    • Opportunity services
    • Viwanda na Biashara
      • New menu item
    • Madini
    • Uvuvi
    • EQUIP-TANZANIA
    • FURSA ZA UWEKEZAJI
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Tafiti
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

RC CHACHA AZINDUA MASHINDANO YA UMITASHUMTA NA UMISSETA MKOA WA TABORA, ATOA WITO WA KULINDA NDOTO ZA WATOTO.

Posted on: May 19th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Mhe. Paulo Chacha, ameongoza  uzinduzi wa mashindano ya michezo ya UMITASHUMTA na UMISSETA ngazi ya mkoa, katika hafla iliyofanyika Mei 19, 2025 katika viwanja vya michezo vya shule ya wavulana Tabora. Hafla hiyo ilihudhuriwa na wanamichezo, viongozi wa elimu, wadau wa maendeleo, walimu na wazazi kutoka halmashauri zote nane za mkoa wa Tabora.

Akimkaribisha mgeni rasmi, Katibu Tawala Msaidizi anayesimamia elimu, Bi. Upendo Rweyemamu, alimshukuru Mheshimiwa Chacha kwa kujitoa kwa dhati kuimarisha elimu na ustawi wa wanafunzi mkoani humo.

“Wewe ni mlezi wa kweli wa vijana wetu. Umekuwa mstari wa mbele kupambana na vitendo vyote vya ukatili dhidi ya watoto. Tunakuombea afya njema ili uendelee kuwa taa ya mkoa wetu,” alisema Bi. Rweyemamu.

Aidha, aliwashukuru wadau mbalimbali waliowezesha kufanikisha mashindano hayo, akiwataja Maafisa ElimuWilaya,Tapsha, Tahossa, Benki ya NMB, Umoja wa Maafisa Elimu Kata, na walimu wote kwa ujumla kwa ushirikiano wao wa hali na mali.

Katika hotuba yake, Mheshimiwa Chacha aliwapongeza wanamichezo wa UMITASHUMTA kwa kushika nafasi ya pili kitaifa kwa mwaka uliopita, akiwahimiza kuendeleza juhudi ili mkoa wa Tabora uibuke kidedea kwenye mashindano ya mwaka huu yatakayofanyika mkoani Iringa.

“Mimi nitafia barabarani kwa ajili ya kulinda ndoto za watoto. Tuwalinde watoto wetu dhidi ya ukatili wa aina yoyote. Tukiona dalili, tuchukue hatua. Tusiwafumbie macho wanaoleta madhara kwa watoto,” alisisitiza Mhe. Chacha.

Alitoa onyo kali kwa watu wasiowaheshimu watoto, akisema wazi: “Shuleni hakuna mwanamke, kuna watoto wa kike tu. Watoto wanapaswa kulindwa na kulelewa tu na wala si kutendewa vinginevyo.”

Aidha, aliwataka walimu wanaosimamia mashindano kuwa waadilifu na kuwatambua wanafunzi kwa vipaji vyao badala ya upendeleo:

Mashindano ya UMITASHUMTA yanayoshirikisha michezo kama mpira wa miguu,mikono, pete, wavu pamoja na sanaa za maonesho yamepangwa kufanyika kwa siku tano kuanzia Mei 17 hadi 22, 2025. Kwa upande wa mashindano ya UMISSETA, yatashika kasi kuanzia Juni 2 hadi Juni 6, 2025.

Zaidi ya wanafunzi 940 wanashiriki katika mashindano haya, wakiwemo wavulana 459, wasichana 481, na walimu, walezi pamoja na waratibu 97.

Mashindano haya yanaendeshwa chini ya usimamizi wa Wizara tatu: Wizara ya  Ofisi ya Rais TAMISEMI, Elimu, na Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo.

Mashindano hayo ya UMITASHUMTA NA UMISSETA yababebwa na Kauli mbiu ya mwaka huu isemayo “Viongozi Bora ni Msingi wa Maendeleo ya Taaluma, Sanaa na Michezo – Shiriki Uchaguzi Mkuu 2025 kwa Amani na Utulivu.”

.

Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 18, 2023
  • SIKU YA KIMATAIFA YA WANAWAKE MACHI 8 March 07, 2024
  • BEI ELEKEZI YA MBOLEA YA CAN KWA KAMPUNI YA YARA June 15, 2022
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MITAALA YA ELIMU TANZANIA BARA March 23, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • RC CHACHA AZINDUA MASHINDANO YA UMITASHUMTA NA UMISSETA MKOA WA TABORA, ATOA WITO WA KULINDA NDOTO ZA WATOTO.

    May 19, 2025
  • TABORA YAADHIMISHA SIKU YA KIMATAIFA YA FAMILIA KWA KUTOA WITO WA MALEZI BORA NA KUPINGA UKATILI.

    May 15, 2025
  • WIZARA YA AFYA NA OFISI YA MKUU WA MKOA WA TABORA YAENDESHA KIKAO ELEKEZI CHA MREJESHO WA MAFUNZO NA MAPITIO YA AFYA YA MAMA NA MTOTO.

    May 14, 2025
  • JESHI LA POLISI TABORA LAPATA MAGARI 6 MAPYA KWA AJILI YA KUIMARISHA USALAMA WA RAIA

    May 12, 2025
  • Angalia zote

Video

VIJANA WAKAA MEZA MOJA NA RC MKOA WA TABORA
video nyingine

Viungio vya Haraka

  • Maelezo na fomu ya ahadi ya uadilifu kwa watumishi wa umma
  • Guidelines for the use of ICT in government
  • Agriculture
  • MALALAMIKO,PONGEZI NA MAONI INGIA HAPA
  • Bofya hapa Eoffice

Tovuti Muhimu

  • Ikulu
  • Ofisi ya Rais-Tamisemi
  • Ofisi ya Rais-Utumishi
  • SALARYSLIP
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tabora

    S.L.P: 25 Tabora

    Simu: 026 2604058

    Mobile:

    Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa mara
    • Service
    • owner

Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa