Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian amelitaka Baraza la Madiwani kwa kutumia wataalamu wa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, kuangalia namna ya kufanya mabadiliko kwenye uwekezaji wa asali ili wazalishaji wanufaike,“Mkurugenzi hakikisha kiwanda kinaanza kufanya kazi kuepuka hasara ya uchakavu kwa mitambo iliyowekwa ili kuinua kipato cha wananchi Kupitia asali wanayovuna”.
Aidha, kufuatia kumiminika kwa miradi mingi ya maendeleo Mkoani Tabora, Mkuu wa Mkoa wa Tabora ameungana na Baraza la Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge kumpongeza Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa miaka miwili ya uongozi wake Mkoa umefanikiwa kwenye sekta mbalimbali zote.
Amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo kusimamia makato ya watumishi na kuhakikisha fedha hizo zinafikishwa kwenye mifuko inayotambulika. “Makato ya fedha za Watumishi ambazo hazikupelekwa kwenye Taasisi husika, mfano Halmashauri zetu zinadaiwa na mfuko wa hifadhi ya jamii (PSSSF), hivyo kusababisha usumbufu kwa wastaafu kutokulipwa mafao yao kwa wakati” Alisema Mkuu wa Mkoa.
Ameikumbusha halmashauri hiyo kutenga fedha za mikopo ya asilimia 10 na kuhakikisha mikopo hiyo inarejeshwa kwa wakati. · “Halmashauri ihakikishe inaendelea kutenga asilimia 10 kwa ajili ya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu kama sheria inavyoelekeza wakati tukisubiri maelekezo ya Serikali”
Haya yamejili leo Juni 12, 2023 wakati Mkuu wa mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt Batilda Salha Burian alipohudhuria Kikao Maalum cha Baraza la Madiwani Halmashauri ya Manispaa ya Tabora cha kupokea taarifa ya mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali iliyoishia Juni 30, 2022.
Tabora
S.L.P: 25 Tabora
Simu: 026 2604058
Mobile:
Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz
Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa