NA TIGANYA VINCENT
MKUU wa Mkoa wa Tabora Balozi Dkt.Batilda Buriani ameagiza Uongozi wa Wilaya ya Igunga kuwandoa wavamizi wa chanzo cha maji katika Bwawa la Mwamapuli liliko katika Kijiji cha Mwanzugi Wilayani Igunga
Alisema wavamizi hao wanaendesha shughuli za kilimo ambacho kinasababisha mchanga kuelekea katika Bwawa hilo na kutishia uendelevu wake.
Balozi Dkt. Batilda alitoa kauli hiyo jana mjini Igunga wakati wa ukaguzi wa mradi mkubwa wa kilimo cha umwagiliaji wa mpunga katika Bwawa la Mwmapuli.
Alisema kuwa Bwawa hilo ni muhimu kwa uzalishaji wa zao la mpunga kwa Mkoa wa Tabora , matumizi ya maji na viumbe kama vile samaki.
Balozi Dkt.Batilda alisema kutokana na kilimo katika chanzo kimesababisha mchanga kipindi cha masika kuelekea katika Bwawa hilo na kupunuza kina cha maji.
Awali Mwenyekiti wa Ushirika wa Wakulima wa Mpunga wa Mwamwapuli(Mwanzugi) Ramdhani Muna alimuomba Mkuu wa Mkoa kutumia vyombo vya dola kuwaondoa wavamizi katika eneo la Nguvu moja kwa sababu wanasababisha kina cha maji kupungua kwa kusababisha mchanga kuingia katika Bwawa .
Alisema sanjari hilo amemuomba Mkuu huyo wa Mkoa kutatua tatizo la wafugaji ambao wamekuwa wakiingiza mifugo katika mashamba ya wakulima na kuharibu miundombinu ya umwagiliaji.
Awali Afisa Kilimo wa Wilaya ya Igunga Grace Mkunda alisema mradi wa umwagilaji wa mwamapuli una ukubwa wa Hekta 630 zinazomikiwa na wakulima 970.
Alisema hekta hizo na una uwezo wa kuzalisha kiasi cha zaidi ya tani 5,000 kwa mwaka za mpunga.
Katika hatua nyingine Mkuu wa Mkoa wa Tabora ameagiza wasimamizi na Maafisa Ugani na Kilimo wa mradi wa kilimo cha umwagiliaji cha Mwamapuli kusaidia wakulima wote wa eneo hilo waweze kuzalisha maguni zaidi ya 80 katika ekari moja.
Tabora
S.L.P: 25 Tabora
Simu: 026 2604058
Mobile:
Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz
Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa