Mkuu wa Mkoa wa Tabora Balozi Dkt. Batilda Buriani amekagua maendeleo ya ujenzi wa barabara ya Usesula hadi Koga yenye urefu wa Kilometa 132 inayounganisha Mkoa wa Tabora na Katavi.
Ukaguzi huo umefanyika jana kwa lengo la kuangalia maendeleo ya ujenzi wa vipande mbalimbali vya barabara hiyo.
Aliwataka Wakandarasi kuongeza kasi kwa kuwa barabara hiyo ni muhimu kwa maendeleo ya Mkoa wa Tabora na Katavi.
Balozi Dkt. Batilda alisema kukamilika kwa barabara hiyo kutatoa fursa kwa wakulima na wafanyabiashara kuyafikisha mazao katika masoko bila matatizo.
Aidha Mkuu huyo wa Mkoa wa Tabora aliwaonya wananchi wenye tabia kuiba alama za barabara kuacha kwa kuwa Serikali ikawakamata itawachukulia hatua kali za kisheria.
Balozi Dkt. Batilda aliwataka wakazi walipo kando kando ya barabara zote kutoa taarifa kwa watu ambao wamekuwa wakiiba alama za barabara.
Akisoma taarifa ya ujenzi, Mhandisi Nurdin Muhungo amesema Mradi huo wa Ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami umeghalimu shilingi bilioni 158.8.
Alisema ujenzi wake umefikia asilimia 87.2 na kuongeza kuwa barabara hiyo inatarajiwa kukamilika ndani ya mwaka huu .
Naye Mkuu wa Kitengo cha Matengenezo ya Barabara na Madaraja TANROADS Mkoa wa Tabora Raphael Mlimaji aliiomba Serikali kuwachukulia hatua watu wanaong’oa alama za barabara kwa kuwa wamesabisha hasara kwa Serikali.
Alisema baadhi ya ajali zimetokana na kung’olewa kwa alama za barabara na kuwafanya madreva kutokuwa na uelewa wa jinsi barabara ilivyo.
Katika hatua nyingine Mkuu wa Mkoa wa Tabora akizungumza na wakazi wa Kata ya Ipole Wilayani Sikonge amewataka kuendelea na taratibu za kujikinga na UVIKO 19 na kuwasisitiza kuchanja wananchi walio katika makundi maalumu ya viapumbele kwa walio hiari kuchanja.
Tabora
S.L.P: 25 Tabora
Simu: 026 2604058
Mobile:
Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz
Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa