Akihutubia Baraza la Madiwani katika Halmashauri ya Mji Nzega, Mkuu wa mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt Batilda Salha Burian amelipongeza baraza la madiwani kwa kuhakikisha Halmashauri imepata hati safi. Alisema “kipekee napenda kuwapongeza madiwani wote, mkurugenzi na wataalamu wote wa Halmashauri kwa kupata hati safi”
Aidha, amesisitiza utolewaji wa elimu kuhusu mfumo wa TAUSI ili kurahisisha shughuli mbalimbali za kiserikali kupitia Halmashauri zetu. Alisema kuwa “Bado mfumo huu una changamoto kwenye matumizi yake, hivyo tutoe elimu kwa umma kupitia vyombo vya habari ili kuhakikisha elimu inawafikia Wananchi wote na kwa urahisi zaidi, kwani serikali imetumia fedha nyingi sana kutengeneza mfumo huu wa TAUSI.”
Ameitaka Halmashauri hiyo kuhakikisha usajili wa mashine za POS unazingatiwa ili kuhakikisha fedha zote za serikali zinakusanywa kupitia mfumo uliowekwa. . Na amewasisitiza wasimamizi wa miradi ya serikali kutokufanya malipo bila kufuata taratibu zilizowekwa.
Aidha, Dkt Batilda Burian ameitaka Halmashauri ya Mji wa Nzega kutenga mikopo ya 10% na kuhakikisha mikopo hiyo inarejeshwa kwa wakati ili Halmashauri iweze kujiendesha. Alisema “Halmashauri ihakikishe inaendelea kutenga asilimia 10 kwa ajili ya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu kama sheria inavyoelekeza wakati tukisubiri maelekezo ya Serikali.”
Tabora
S.L.P: 25 Tabora
Simu: 026 2604058
Mobile:
Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz
Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa