Akitoa hotuba yake Mhe. Mkuu wa Mkoa amemuhakikishia Jaji Mfawidhi Dkt. Juma, serikali itaendelea kushirikiana na mahakama kama moja ya muhimiri muhimu katika taifa letu katika utoaji wa haki kwa mujibu wa Sheria zilizowekwa.
Sambamba na hilo Mhe. Batilda ameipongeza mahakama kwa kuwashirikisha kikamilifu wananchi katika kutoa mawazo yao katika kukamilisha mchakato wa Haki Jinai kama moja ya msingi muhimu wa kuwajibika kwa wananchi kwa mujibu wa sheria.
Kwa upanda wake, Mhe. Dkt. Adam Juma Mambi Jaji Mkuu wa Mahakama kuu Tabora amemshukuru Mkuu wa Mkoa wa Tabora na kutoa shukrani kwa serikali kwa kutoa ushirikiano katika kukamilisha mchakato wa haki jinai, na kumuahidi Mkuu wa Mkoa, mahakama itaendelea kushirikiana na serikali katika kutoa huduma za kimahakama kwa wananchi ili kuendana na kauli mbiu ya maadhimisho hayo.
Maadhimisho ya siku ya Sheria nchini yamefikia tamati leo Februari 1, 2024 yakiashiria kuanza kwa mwaka mpya wa kimahakama na yenye kauli mbiu isemayo “Umuhimu wa dhana ya Haki Jinai kwa Ustawi wa Taifa: Nafasi ya Mahakama na Wadau katika kuboresha Mfumo Jumuhishi wa Haki Jinai”
Tabora
S.L.P: 25 Tabora
Simu: 026 2604058
Mobile:
Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz
Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa