Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian ameungana na mamia ya wananchi wa Tabora kushiriki kwenye maadhimisho ya Siku ya UKIMWI duniani ambayo kwa ngazi ya Mkoa yanafanyika Wilayani Urambo. Kauli mbiu ya mwaka huu inasema “Jamii Iongoeze Kutokomeza UKIMWI”
Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian akiwasili katika viwanja vya Wananchi Squire vilivyopo Wilayani Urambo na kupokelewa na baadhi ya viongozi kutoka Wilaya ya Urambo, tayari kushiriki kwenye maadhimisho ya Siku ya UKIMWI duniani ambayo kwa ngazi ya Mkoa yanafanyika Wilayani Urambo.
Baadhi ya wananchi kutoka Wilaya ya Urambo wamejitokeza na kushiriki kwenye maadhimisho ya Siku ya UKIMWI duniani ambayo kwa ngazi ya Mkoa yanafanyika Wilayani Urambo, kwenye Viwanja vya Wananchi Squire.
Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian akikagua, kujionea na kupata maelezo kutoka kwa wataalamu wa masuala ya Afya kwenye mabanda yaliyokuwepo katika Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani , yakihusisha wadau mbalimbali wakiwemo MDH.
Baadhi ya wananchi wakijitokeza sehemu za kutolea huduma za afya kwenye mabanda zikiwemo uchangiaji wa damu, upimaji wa VVU, upimaji wa Maralia na utolewaji w ushauri na nasaa kuhusiana na masuala ya Afya, kwenye Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani .
Kwa niaba ya Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tabora Ndugu. Joseph Kasiga akiwasilisha taarifa ya maendeleo ya Afya hususani hali ya maambukizi ya VVU Kwa Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian kwenye Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani.
Kwa niaba ya Katibu Tawala Mkoa wa Tabora Ndugu. Innocent Nsenna Katibu Tawala Wilaya ya Urambo akitoa salamu za Mkoa na kisha kumkaribisha Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian kwa ajili ya kuwahutubia mamia ya wananchi waliojitokeza kwenye Mahadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani.
Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian akihutubia mamia ya wananchi kutoka Wilaya ya Urambo na maeneo ya jirani kwenye Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani ambayo kwa ngazi ya Mkoa yamefanyika Wilayani Urambo, kwenye viwanja vya Wananchi Squire, Disemba 1, 2023.
Ambapo sehemu kubwa ya hotuba yake, Mhe. Mkuu wa Mkoa ameeleza mafanikio makubwa yaliofikiwa kwenye sekta ya afya kwa kipindi cha miaka miwili ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano, hususani ujenzi wa hospitali mpya za wilaya, vituo vya afya, majengo ya dharura na majengo ya wagojwa wenye mahitaji maalumu.
Pia, Dkt. Batilda ameelezea, mwamko wa wananchi wa mkoa wa Tabora katika suala la upimaji wa VVU kwa hiari jambo ambalo limechangia kwa kiasi kikubwa kwa Serikali kuweka mikakati ya kupambana na maambukizi mapya.
Aidha, Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa amebainisha changamoto ya wimbi la vijana wanaojihusisha na vitendo vya ngono ambao wameongeza kasi ya kusambaa kwa maambukizi ya VVU na kuhatarisha maisha ya watanzania. Na kutoa rai kwa watanzania kuendelea kujikinga na VVU kwani bado ugonjwa huu upo.
Wananchi wa Wilaya ya Urambo na maeneo ya jirani wakisikiliza hotuba ya Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian aliyoihutubia kwenye Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani.
Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian akiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi mbalimbali kutoka Wilaya Ya Urambo, mara baada ya kutoa hotuba yake kwenye Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani
Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian akiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi mbalimbali wa kisiasa kutoka Wilaya Ya Urambo, mara baada ya kutoa hotuba yake kwenye Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani
Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian akiwa kwenye picha ya pamoja na kamati ya Usalama ya Wilaya ya Urambo mara baada ya kutoa hotuba yake kwenye Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani
Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian akiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi wa dini mbalimbali mbalimbali kutoka Wilaya Ya Urambo, mara baada ya kutoa hotuba yake kwenye Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani
Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian akiwa kwenye picha ya pamoja na wanafunzi kutoka shule mbalimbali mara baada ya kutoa hotuba yake kwenye Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani
Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian akiwa kwenye picha ya pamoja na taasisi mbalimbali zisizo za kiserikali mara baada ya kutoa hotuba yake kwenye Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani .
Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian akiwa kwenye picha ya pamoja na wataalam wa Afya na Ustawi wa Jamii kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa mara baada ya kutoa hotuba yake kwenye Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani
Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian akiondoka na kuwaaga wananchi wa Wilaya ya Urambo na maeneo ya jirani kwenye viwanja vya Wananchi Squire mara baada ya kumaliza kwa Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani. ambayo kwa ngazi ya Mkoa yalifanyika Wilayani Urambo, kwenye viwanja vya Wananchi Squire, Disemba 1, 2023.
Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kwa ngazi ya Mkoa yanafanyika Wilayani Urambo wakati huo huo maadhimisho haya kwa ngazi ya taifa yanafanyika Mkoani Morogoro, ambayo yalifunguliwa Novemba 24, 2023.
Tabora
S.L.P: 25 Tabora
Simu: 026 2604058
Mobile:
Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz
Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa