MKUU wa Mkoa wa Tabora Balozi Dkt.Batilda Buriani wadau wakiwemo Wafanyabiashara kusaidia timu za Mpira wa Miguu ili walau kuwepo zinazocheza Ligi.
Alisema Tabora inahistoria kubwa katika michezo na uzalishaji wa Vipaji wa Wachezaji ambao baadhi yao walifanikiwa kuchezea Timu ya Simba na Yanga
Balozi Dkt. Batilda alitoa kauli hiyo jana mjini hapa wakati wa uzinduzi wa Baraza la Biashara la Manispaa ya Tabora.
Alisema bado ya kuwa na Wachezaji kutoka Tabora waliofanya vizuri pia kulikuwepo na timu mbalimbali ambazo zilisaidia kuutangaza Mkoa.
Balozi Dkt. Batilda alisema imefika Wadau mbalimbali wakakakutana na kuangilia uwezekano wa kiziongezea nguvu timu zilizopo ili ziweze kupanda Daraja.
Mkuu huyo wa Mkoa alisema Ofisi yake iko wazi katika kuweka mazingira wezeshi ambao yatawafanya Wachezaji kufanya vizuri katika mashindano mbalimbali.
Alisema zitakapofanikiwa zitasaidia kukuza uchumiwa wa Mkoa wa Tabora kutokana na wageni ambao watakuja kuangalia Ligi.
Tabora
S.L.P: 25 Tabora
Simu: 026 2604058
Mobile:
Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz
Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa