• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Nukushi ya malalamiko |
TABORA REGION ADMINISTRATIVE SECRETARY

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi Ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tabora

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Biashara
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo Cha Mawasiliano
    • Muundo
  • Wilaya
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Wilaya ya Urambo
    • Wilaya ya Igunga
    • Wilaya ya Uyui
    • Wilaya ya Kaliua
    • Wilaya ya Sikonge
    • Wilaya ya Nzega
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Tabora
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Halmashauri ya Wilaya ya Igunga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua
    • Halmashauri ya Wilaya Urambo
    • Halmashauri ya Mji wa Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya Sikonge
  • Fursa za Uwekezaji
    • Miombo Project
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi inayoendelea
    • Kilimo
      • Miombo Project
        • Miradi iliyokamilika
        • Miradi inayoendelea
    • Mifugo
    • Opportunity services
    • Viwanda na Biashara
      • New menu item
    • Madini
    • Uvuvi
    • EQUIP-TANZANIA
    • FURSA ZA UWEKEZAJI
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Tafiti
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

RC TABORA AWAONYA WATU WANAOCHUKUA MBEGU ZA PAMBA KWA WAKULIMA NA KUPELEKA KATIKA MATUMIZI MENGINE

Posted on: November 27th, 2020

MKUU wa Wilaya na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Igunga wametakiwa kuwasaka na kuwamata wafanyabiashara wasiokuwa na waadilifu ambao wamekuwa wakichukua mbegu za pamba na kuzipeleka katika matumizi ambayo hayakusudiwa.

Kauli hiyo imetolewa  na Mkuu wa Mkoa wa Tabora Dkt. Philemon Sengati wakati wa uzinduzi wa msimu wa kilimo uliyofanyika wilayani Igunga.

Alisema watu hao sio wazalendo na hawataki mema wakulima kwa kuwa wanataka kuhujumu kilimo cha pamba katika Wilaya ya Igunga na Mkoa wa Tabora kwa ujumla.

“Wafanyabiashara wa aina hiyo ni wahujumu uchumi na wahujumu maendeleo na sisi kama Mkoa tutaendelea kuwasaka na kuwashughulikia usiku na mchana kwa kuzingatia Sheria” alisema.

Aidha Dkt. Sengati alisema sanjari na hilo aliwataka  kuhakikisha kuwa mbolea zinazotolewa zinazouzwa kwa bei elekezi ambayo ni shilingi 57,000/= kwa mfuko wa kilo 50 na sio zaidi ya hapo.

Mkurugenzi wa Huduma za Usimamizi wa Bodi ya Pamba nchini James Shime alisema kuna baadhi ya watu ambao wakiwarubuni wakulima na kununua mbegu walizopatiwa na Bodi na kuzipeleka katika matumizi mengine kama vile usindikaji wa mafuta.

Alisema watu hao wanafanya hivyo ili kutengeneza upungufu kwa wakulima wakati sio kweli kwani Bodi imeshasambaza tani 10,000 za mbegu kati tani 11,000 zinatakiwa nchi nzima.

Shimbe alisema watu hao ni wahujumu uchumi na baadhi watu wameshakamatwa wakiwa wamepakia mbegu na msako unaendelea.

Naye Afisa Kilimo kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tabora Modest Kaijage alisema ni hatari kutumia mbegu za pamba kwa ajili ya kuzalisha mafuta kwa kuwa zinakuwa zimewekewa dawa ambayo inaweza kuwa na athari kwa watumiaji.

Wakati huo huo Mkuu huyo wa Mkoa amewaonya wakulima wa pamba ambao hawang’oa masalia ya pamba na kutayarisha mashamba yao kuwa Serikali itawachukulia hatua kwa mujibu Sheria.

Alisema kuendelea kuacha masalia katika shamba ni kutenda kosa na mhusika anaweza kushitakiwa na kuwataka kuyaondoa haraka.

Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 18, 2023
  • SIKU YA KIMATAIFA YA WANAWAKE MACHI 8 March 07, 2024
  • BEI ELEKEZI YA MBOLEA YA CAN KWA KAMPUNI YA YARA June 15, 2022
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MITAALA YA ELIMU TANZANIA BARA March 23, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • BARAZA LA BIASHARA MKOA WA TABORA LADHAMIRIA KULETA MAGEUZI KATIKA KUBORESHA MAZINGIRA YA BIASHARA NA UWEKEZAJI KWA WANANCHI

    May 21, 2025
  • VIONGOZI WA MIKOA YA TABORA NA KIGOMA WAFANYA KIKAO CHA MAANDALIZI KUELEKEA MAONESHO YA SIKUKUU YA WAKULIMA NANE NANE 2025

    May 20, 2025
  • RC CHACHA AZINDUA MASHINDANO YA UMITASHUMTA NA UMISSETA MKOA WA TABORA, ATOA WITO WA KULINDA NDOTO ZA WATOTO.

    May 19, 2025
  • TABORA YAADHIMISHA SIKU YA KIMATAIFA YA FAMILIA KWA KUTOA WITO WA MALEZI BORA NA KUPINGA UKATILI.

    May 15, 2025
  • Angalia zote

Video

VIJANA WAKAA MEZA MOJA NA RC MKOA WA TABORA
video nyingine

Viungio vya Haraka

  • Maelezo na fomu ya ahadi ya uadilifu kwa watumishi wa umma
  • Guidelines for the use of ICT in government
  • Agriculture
  • MALALAMIKO,PONGEZI NA MAONI INGIA HAPA
  • Bofya hapa Eoffice

Tovuti Muhimu

  • Ikulu
  • Ofisi ya Rais-Tamisemi
  • Ofisi ya Rais-Utumishi
  • SALARYSLIP
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tabora

    S.L.P: 25 Tabora

    Simu: 026 2604058

    Mobile:

    Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa mara
    • Service
    • owner

Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa