Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian amewataka Wanatabora na Watanzania kwa ujumla kuchangamkia fursa za miradi ambayo imezinduliwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassani, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alipofanya ziara yake Mkoani Tabora. Ameyasema hayo leo Oktoba 20, 2023 alipokutana na waandishi wa Habari kumshukuru Ofisini kwake.
“Napenda kutoa wito kwa wanatabora na watanzania wote kuchangamkia fursa kwenye miradi ambayo Rais wetu mpendwa ameizindua alipofanya ziara yake Mkoani Tabora”
Dkt. Batilda ameeleza kuwa, tayari Mkoa umeshaweka mikakati kuhakikisha mradi wa chuo cha VETA uliopo Wilayani Igunga unawafaidisha vijana kupitia mipango mbalimbali itakayowekwa ili kuwapa kipaumbele vijana.
“Muheshimiwa Rais ameelekeza kuwasimamia vijana, na sisi kama viongozi wa Mkoa tutahakikisha miradi iliyozinduliwa inawafaidisha vijana kupitia program mbalimbali ikiwemo Jenga Kesho Iliyo Bora (BBT)”
Kwa upande mwingine, Mkuu wa mkoa amekiri Mkoa kuwa na changamoto ya vijana kutochangamkia fursa zinazotolewa kwa vijana hususani kwenye mafunzo ya ufundi na kuwataka vijana kuchangamkia fursa hizo.
“Kunzia Januari chuo kile ambacho Muheshimiwa Rais amekizindua kitaanza kazi, kitaanza kusomesha masuala ya ufundi kwa kozi fupi fupi na kozi ndefu na kuna mabweni pale ya Watoto wa kile na Watoto wa kiume, na naomba fursa hii tuanze kuipata watu wa Tabora na nitashangaa kuona watu wa mikoa mingine wakianza kufaidika” Alisema Mkuu wa Mkoa
Sambamba na hilo, Mkuu wa Mkoa amemshukuru Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassani, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa ziara yake Mkoani Tabora na kuzindua miradi mikubwa ambayo kwa hakika imekuwa na faida kubwa sana kwa Wanatabora na Watanzania kwa ujumla”
“Nitoe shukrani zangu kwa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassani, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa ziara yake hapa mkoani kwetu ambayo kwa kweli imekuwa na faida kubwa kwa mkoa na taifa kwa ujumla, na miradi yote aliyozindua inagusa jamii moja kwa moja” alisema Dkt. Batilda
Aidha Mhe. Dkt Batilda amemuhakikishia Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassani, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kusimamia na kutekelez maelekezo yote aliyoyatoa wakati wa ziara yake Mkoani Tabora.
“Nipende kumuhakikishia Muheshimiwa Rais kuwa, maelekezo yote aliyotupatia wakati wa ziara yake, tunayafanyia kazi ili kuhakikisha miradi yote aliyozindua inakuwa na tija kwa Wanatabora na Watanzania kwa ujumla” alisema Mkuu wa Mkoa
Ikumbukwe kuwa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassani, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alikuwa na ziara ya siku mbili Mkoani Tabora, na kutembelea Wilaya ya Igunga na Nzega na kuzindua miradi mikubwa miwili ukiwemo mradi wa Chuo Cha Veta uliopo wilayani Igunga. Na mradi wa Umwagiliaji wa Center Pivot uliopo Wilayani Igunga.
#Kazi Iendelee
Tabora
S.L.P: 25 Tabora
Simu: 026 2604058
Mobile:
Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz
Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa