Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt.Batilda Salha Burian amezitaka Halamshauri zote Mkoani Tabora kuhakikisha zinakuwa na kalakana ya kutengeneza madawati ili kuhakikisha miradi ya ujenzi wa miundombinu ya elimu inakamilika kwa wakati pasipo kusubiri wazabuni.Ameyasema hayo leo Julai 13, 2023 alipofanya ziara ya ukaguzi wa miradi ya BOOST wilaya ya Uyui na Igunga.
“niwaombe Wakurugenzi wote kwenye Halmshauri zetu, tuhakikishe tuwe na kalakana za kutengeza madawati ili kuepukana na changamoto zinazojitokeza za ucheleweshaji wa madawati kutoka kwa wazabuni na kusababisha madarasa kukamilika bila madawati”
Akikagua miradi hiyo, Mkuu wa mkoa wa Tabora amempongeza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Nzega Ndugu Shomari Mndolwa kwa kukamilisha mradi wa ujenzi wa Shule mpya ya Msingi Uwanja wa Ndege kwa asilimia kubwa na wenye ubora.
“ Napenda kutoa pongezi zangu kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Nzega kwa kufanya kazi usiku na mchana na kuhakikisha ujenzi wa shule hii unakamilika tena ukiwa na viwango vizuri, na niwaombe Wakurugenzi wengine waige mfano huu ili kwenye Mkoa wetu uwe unakamilisha miradi kwa wakati”
Leo Julai 13, 2023 Mkuu wa Mkoa amekagua jumla ya miradi mitano (5) kwa Wilaya ya Uyui na Nzega ambapo miradi mitatu (3) ni ya elimu na miwili (2) ni miradi ya afya. Kesho Julai 14, atakagua miradi minne (4) Wilayani Igunga.
Tabora
S.L.P: 25 Tabora
Simu: 026 2604058
Mobile:
Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz
Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa