Kufuatia ucheleweshwaji wa malipo kwa wakulima wa Tumbaku kwa zaidi ya Siku 40 baada ya soko kufanyika, Mkuu wa mkoa wa Tabora Mhe. Dkt. Batilda Salha Burian ameiagiza kampuni ya ununuzi wa Tumbaku ya VOEDSEL kuhakikisha wanawalipa wakulima madeni yao ndani ya siku saba.
Akiongea na wawakilishi wa kampuni mapema leo Juni 9, 2023 kwenye Ukumbi mdogo wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Dkt. Batilda Salh Burin ameitaka kampuni hiyo kulipa madeni yake ya Bilioni 20 wanazodaiwa na wakulima. “Kuna sababu gani ya kuwatesa wakulima wa tumbaku siku 40 mpaka leo mkulima hajalipwa, hatutaki kurudi tulipotoka” alisisitiza Mkuu wa Mkoa wa Tabora.
Aidha, Dkt. Batilda ameleza kuwa, Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alishaagiza kuwa malipo ya wakulima yafanyike haraka ndani ya siku tatu (3) na kwamba kama Mkoa tutahakikisha tunasimamia maagizo hayo kikamilifu. Haipendezi kuona kama serikali haifanyi kazi wakati tayari Serikali ilishaweka mazingira wezeshi kwa wakulima wa tumbaku” alisema Mkuu wa mkoa wa Tabora.
Soko la tumbaku la 2022/2023 lilifunguliwa na Mkuu wa mkoa wa Tabora Mhe. Dkt. Batilda Salha Burian mnamo Aprili 25, 2023.
Tabora
S.L.P: 25 Tabora
Simu: 026 2604058
Mobile:
Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz
Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa