• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Nukushi ya malalamiko |
TABORA REGION ADMINISTRATIVE SECRETARY

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi Ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tabora

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Biashara
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo Cha Mawasiliano
    • Muundo
  • Wilaya
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Wilaya ya Urambo
    • Wilaya ya Igunga
    • Wilaya ya Uyui
    • Wilaya ya Kaliua
    • Wilaya ya Sikonge
    • Wilaya ya Nzega
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Tabora
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Halmashauri ya Wilaya ya Igunga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua
    • Halmashauri ya Wilaya Urambo
    • Halmashauri ya Mji wa Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya Sikonge
  • Fursa za Uwekezaji
    • Miombo Project
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi inayoendelea
    • Kilimo
      • Miombo Project
        • Miradi iliyokamilika
        • Miradi inayoendelea
    • Mifugo
    • Opportunity services
    • Viwanda na Biashara
      • New menu item
    • Madini
    • Uvuvi
    • EQUIP-TANZANIA
    • FURSA ZA UWEKEZAJI
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Tafiti
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

RC TABORA “MAGARI NA PIKIPIKI YATUMIKE KWA SHUGHULI ZILIZOKUSUDIWA”

Posted on: January 10th, 2024
  • Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian amewataka watendaji wote wa Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) mkoani Tabora kuhakikisha magari na pikipiki walizopewa zinatumika kwa shughuli zilizokusudiwa ili kuhakikisha wananchi wanafikiwa na huduma za maji kikamilifu. Ameyasema hayo leo Januari 10, 2024 alipokuwa anakabidhi magari matano (5) na pikipiki 45 kwa watendaji wa RUWASA.

Mkuu wa Mkoa ameendelea kusema kuwa, anamshukuru Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya  kwa kuendelea kutenga fedha ambazo zinaendelea kukamilisha miradi mbalimbali ikiwemo ununuaji wa zana za usafirishaji.

“Rais wetu kipenzi ameamua kutoa kiasi cha Shilingi milioni 934.5 kwa ajili ya kugharamia ununuzi wa vyombo vya usafiri ikijumuisha magari 5 yenye thamani ya Shilingi milioni 802.4 na pikipiki 48 zenye thamani ya Shilingi milioni 132 zitakazoenda kuongeza nguvu katika usimamizi na uendeshaji wa miradi ya maji katika Mkoa wetu” alisema Mkuu wa Mkoa.

Sambamba na hilo, Mheshimiwa Batilda ametoa wito kwa wadereva wa Vyombo hivyo kufuata Sheria kikamilifu ili kuepukana na ajali.      

“Madereva wa magari na pikipiki waendeshe kwa kufuata sheria za barabarani ili kuepuka kupata ajali ambazo zinaweza kutokea kama sheria za barabarani hazitofuatwa” alisisitiza Mhe. Batilda

Naye, Meneja wa RUWASA Mkoa wa Tabora Muhandisi Hatari Kipufi amesema kuwa kwa kipindi cha miaka miwili na nusu huduma za maji mkoani Tabora zimeimarika kwa kiasi kikubwa sana ambapo kwa upatikanaji wa maji mijini ni asilimia 75 na vijijini ni asilimia 68 ambapo mpaka kufikia mwaka 2025 upatikanaji wa maji mjini unatarajiwa kufikiwa asilimia 95 na vijiji ni asilimia 85.

Mkuu wa Mkoa wa Tabora amekabidhi magari matano kwa watendaji wa RUWASA, ambapo gari moja amekabidhiwa Meneja wa RUWASA Mkoa wa Tabora na mengine manne wamekabidhiwa Mameneja wa RUWASA wa wilaya ya Igunga, Nzega, Uyui na Sikonge.


MATUKIO KATIKA PICHA

Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian akiwasili karika Ofisi ya RUWASA Mkoa wa Tabora, iliyopo Manispaa ya Tabora kushiriki kwenye hafla ya ugawaji wa vyombo vya usafiri kwa watendaji mbalimbali wanaohudumu kwenye selta ya maji  ikihusisha magari matano (5) na pikipiki arobaini  na tano (45) Januari 10, 2024.

Meneja wa RUWASA Mkoa wa Tabora Muhandisi Hatari Kapufi akitoa taarifa ya maendeleo ya Sekta ya maji Mkoani Tabora kwa Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian kwenye hafla fupi ya ugawaji wa vyombo vya usafiri iliyofanyika katika Ofisi za RUWASA zilizopo Manispaa ya Tabora, Januari 10, 2024.


Kwa niaba ya Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Tabora na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa (MCC), Ndugu Hassan Wakasuvi, Katibu wa Wazazi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Ndugu. Emmanuel Sabuhoro akitoa salamu za Chama Chama cha Mapinduzi katika hafla fupi ya ugawaji wa vyombo vya usafiri iliyofanyika katika Ofisi za RUWASA zilizopo Manispaa ya Tabora, Januari 10, 2024.

Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian akihutubia watumishi wa RUWASA, Jumuhiya za Watumiaji Maji, Wadau wa Sekta ya Afya na Wananchi katika hafla fupi ya ugawaji wa vyombo vya usafiri iliyofanyika katika Ofisi za RUWASA zilizopo Manispaa ya Tabora, Januari 10, 2024.

Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian akikata utepe kuashiria kukamilika kwa hafla ya ugawaji wa vyombo vya usafiri kwa watendaji mbalimbali wanaohudumu kwenye Sekta ya maji  ikihusisha magari matano (5) na pikipiki arobaini  na tano (45) Januari 10, 2024.

Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian akimkabidhi gari jipya aina ya Land Cruiser  Meneja wa RUWASA Mkoa wa Tabora Muhandisi Hatari Kapufi kwenye hafla fupi ya ugawaji wa vyombo vya usafiri iliyofanyika katika Ofisi za RUWASA zilizopo Manispaa ya Tabora, Januari 10, 2024.

Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian akiwakabidhi funguo za magari na pikipikiMameneja wa RUWASA wa Wilaya kwenye hafla fupi ya ugawaji wa vyombo vya usafiri iliyofanyika katika Ofisi za RUWASA zilizopo Manispaa ya Tabora, Januari 10, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian akiwakabidhi funguo za pikipiki baadhi ya viongozi wa Jumuhiya mbalimbali za watumiaji maji kwenye hafla fupi ya ugawaji wa vyombo vya usafiri iliyofanyika katika Ofisi za RUWASA zilizopo Manispaa ya Tabora, Januari 10, 2024


Haya ndio magari matano (5) na pikipiki arobaini na tano (45)  ambazo leo Januari 10, 2024, Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian amezigawa kwa watendaji wa Wakala wa Usambazaji wa Maji na Usafi na Mazingira Vijijini (RUWASA) ngazi ya Mkoa na Wilaya.

Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 18, 2023
  • SIKU YA KIMATAIFA YA WANAWAKE MACHI 8 March 07, 2024
  • BEI ELEKEZI YA MBOLEA YA CAN KWA KAMPUNI YA YARA June 15, 2022
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MITAALA YA ELIMU TANZANIA BARA March 23, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • BARAZA LA BIASHARA MKOA WA TABORA LADHAMIRIA KULETA MAGEUZI KATIKA KUBORESHA MAZINGIRA YA BIASHARA NA UWEKEZAJI KWA WANANCHI

    May 21, 2025
  • VIONGOZI WA MIKOA YA TABORA NA KIGOMA WAFANYA KIKAO CHA MAANDALIZI KUELEKEA MAONESHO YA SIKUKUU YA WAKULIMA NANE NANE 2025

    May 20, 2025
  • RC CHACHA AZINDUA MASHINDANO YA UMITASHUMTA NA UMISSETA MKOA WA TABORA, ATOA WITO WA KULINDA NDOTO ZA WATOTO.

    May 19, 2025
  • TABORA YAADHIMISHA SIKU YA KIMATAIFA YA FAMILIA KWA KUTOA WITO WA MALEZI BORA NA KUPINGA UKATILI.

    May 15, 2025
  • Angalia zote

Video

VIJANA WAKAA MEZA MOJA NA RC MKOA WA TABORA
video nyingine

Viungio vya Haraka

  • Maelezo na fomu ya ahadi ya uadilifu kwa watumishi wa umma
  • Guidelines for the use of ICT in government
  • Agriculture
  • MALALAMIKO,PONGEZI NA MAONI INGIA HAPA
  • Bofya hapa Eoffice

Tovuti Muhimu

  • Ikulu
  • Ofisi ya Rais-Tamisemi
  • Ofisi ya Rais-Utumishi
  • SALARYSLIP
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tabora

    S.L.P: 25 Tabora

    Simu: 026 2604058

    Mobile:

    Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa mara
    • Service
    • owner

Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa