Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian amewataka watendaji wote kuanzia ngazi ya kata hadi mkoa kusimamia Sheria zilizowekwa ili kulinda miundombinu yetu ya barabara. Ameyasema hayo leo Julai 26, 2023 kwenye ufunguzi wa Kikao cha Bodi ya Barabara kilichofanyika katika ukumbi wa Isike Mwanakiyungi.
“Kupia kikao hiki, natoa wito kwa Mamlaka zote za usimamizi kuanzia ngazi za vijiji hadi Mkoa kuendelea kusimamia kikamilifu sheria na taratibu ili kuhakikisha kuwa watu wote watakaobainika kuhujumu miundombinu ya barabara wachukuliwe hatua”
Akitoa hotuba yake, Mkuu wa Mkoa amempongeza na kumshukuru Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutoa fedha ambazo zimetumika katika kuimarisha miundombinu ya barabara.
“Kwa namna ya pekee na kwa heshima kubwa, naomba kuchukuwa nafasi hii kumshukuru na kumpongezi Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa jitihada anazofanya kuimarisha miundombinu mbalimbali nchini”
Sambamba na hilo, Dkt. Batilda Salha Burian amewapongeza watendaji wa ngazi zote kwa kusimamia na kutekeleza miradi yote ikiwemo miradi ya barabara.
“Hakika mnafanya kazi kubwa, mafanikio yote haya yanayoonekana katika Mkoa wetu yanatokana na bidii zenu kwa ujumla, hongereni sana”
Aidha. Mkuu wa Mkoa ameweka wazi changamoto ya uharibu wa miundombinu ya Barabara na kwamba Serikali kupitia TANROAD NA TARURA wanaweka mikakati ya kupambana na uharibifu huo.
“Jitihada mbalimbali zimefanyika kukabiliana na uharibifu huu na jitihada hizo zinaanza kuzaa matunda angalau wizi wa alama na taa za barabarani kwa upande wa TANROADS umepungua kwa mwaka huu”
Tabora
S.L.P: 25 Tabora
Simu: 026 2604058
Mobile:
Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz
Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa