• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Nukushi ya malalamiko |
TABORA REGION ADMINISTRATIVE SECRETARY

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi Ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tabora

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Biashara
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo Cha Mawasiliano
    • Muundo
  • Wilaya
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Wilaya ya Urambo
    • Wilaya ya Igunga
    • Wilaya ya Uyui
    • Wilaya ya Kaliua
    • Wilaya ya Sikonge
    • Wilaya ya Nzega
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Tabora
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Halmashauri ya Wilaya ya Igunga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua
    • Halmashauri ya Wilaya Urambo
    • Halmashauri ya Mji wa Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya Sikonge
  • Fursa za Uwekezaji
    • Miombo Project
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi inayoendelea
    • Kilimo
      • Miombo Project
        • Miradi iliyokamilika
        • Miradi inayoendelea
    • Mifugo
    • Opportunity services
    • Viwanda na Biashara
      • New menu item
    • Madini
    • Uvuvi
    • EQUIP-TANZANIA
    • FURSA ZA UWEKEZAJI
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Tafiti
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

RC TABORA “TUTUMIE TAKWIMU ZA SENSA KWA MAENDELEO YETU”

Posted on: January 18th, 2024
  • Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian amewataka watendaji wote wa serikali mkoani Tabora kuzitumia takwimu na matokeo ya SENSA ya watu na makazi ya mwaka 2022 na takwimu nyingine kwenye mipango ya maendeleo ya mkoa. Ameyasema hayo leo Januari 18, 2024 wakati wa ufungaji wa mafunzo ya matumizi ya matokeo ya SENSA ya watu na makazi ya mwaka 2022 kwa viongozi na makundi mbalimbali yaliofanyika katika ukumbi wa Ristalemi, Manispaa ya Tabora.

 

Alisema “Matokeo ya SENSa ya watu na makazi, SENSA ya majengo na SENSA ya anuani za makazi yawe ndio dira yetu inayotuongoza katika kuandaa na kuhuisha sera, kupanga na kufuatilia utekelezaji wa mipango na program za maendeleo ya mkoa wetu na kutathmini utekelezaji wake”

 

Sambamba na hilo Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa ameeleza kuwa, kupitia SENSA ya watu na makazi ya mwaka 2022, mkoa wa Tabora una idadi ya watu wapatao milioni 3.3 ambapo wanawake ni milioni 1.7 na wanaume ni milioni 1.6 na kuufanya mkoa wa Tabora kushika nafasi ya tatu kitaifa kwa kuwa na idadi kubwa ya watu.

 

Aidha, Mhe. Batilda Burian amebainisha malengo ya mafunzo hayo kuwa ni kujenga  uwezo wa kutafsiri, kuchambua na kuyatumia matokeo ya SENSA katika mpingo mbalimbali ya maendeleo.

  Alisema kuwa “kwa kuwa suala la kupanga mipango ya maendeleo ni shirikishi na linaanzia ngazi ya chini hadi taifa, sisi kama viongozi tuna wajibu wa kuratibu suala zima la upangaji wa maendeleo katika mkoa wetu”

 

Naye, Mwakilishi wa Mtakwimu Mkuu wa Serikali Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) Ndugu. Benedict Mugambi amesema kuwa mafunzo haya yanalengo ya kuwajengea uwezo viongozi wa kiserikali na makundi mbalimbali katika kupanga mipango ya maendeleo kwa kutumia taarifa rasmi zilizopo kwenye matokeo ya SENSA mbalimbal zilizofanyika. 

 

Mfunzo haya ya matumizi ya matokeo ya SENSA ya watu na makazi ya mwaka 2022 yalifunguliwa  rasmi na Mkuu wa Wilaya ya Tabora Mhe. Peter Bura asubuhi ya leo Januari 18, 2024 na yalihusishwa viongozi mbalimbali wa serikali kuanzia kazi ya kata hadi mkoa sambamba na wananchi kutoka kwenye makundi mbalimbali. Mafunzo haya yanafanyika kwa awamu, ambapo kwa mkoa wa Tabora awamu ya kwanza imeanzia wilaya ya Tabora na kumalizikia wilaya ya Uyui Januari 19, 2024.

Mafunzo haya yalienda sambamba na ugawaji wa ramani zenye taarifa kuhusiana na idadi ya watu na makazi ambazo ziligawiwa kwa kuanzia ngazi ya Mkoa hadi ngazi ya kata.

Mwakilishi wa Mtakwimu Mkuu wa Serikali Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) Ndugu. Benedict Mugambi akimkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian, ramani ya Mkoa wa Tabora yenye kuonyesha makazi ya watu na idadi yao mara baada ya Mkuu wa Mkoa kuhutubia kwenye hafla ya ufungaji  wa mafunzo ya usambazaji na matumizi ya matokeo ya SENSA ya watu na makazi kwa viongozi na makundi mbalimbali kutoka Mkoani Tabora, yaliofanyika katika ukumbi wa Ristalemi, Januari 18, 2024

Mkuu wa mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian akimkabidhi Mwakilishi wa Mkuu wa Wilaya ya Tabora, Ramani zenye kuonyesha makazi na idadi ya watu mara baada ya Mkuu wa Mkoa kuhutubia kwenye hafla ya ufungaji  wa mafunzo ya usambazaji na matumizi ya matokeo ya SENSA ya watu na makazi kwa viongozi na makundi mbalimbali kutoka Mkoani Tabora, yaliofanyika katika ukumbi wa Ristalemi, Januari 18, 2024

Mkuu wa mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian akimkabidhi Mwakilishi wa Mkurugenzi Mtendaji wa Manispaa ya Tabora, Ramani zenye kuonyesha makazi na idadi ya watu mara baada ya Mkuu wa Mkoa kuhutubia kwenye hafla ya ufungaji  wa mafunzo ya usambazaji na matumizi ya matokeo ya SENSA ya watu na makazi kwa viongozi na makundi mbalimbali kutoka Mkoani Tabora, yaliofanyika katika ukumbi wa Ristalemi, Januari 18, 2024.

Mkuu wa mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian akiwakabidhi Watendaji wa Kata wa Manispaa ya Tabora Ramani zenye kuonyesha makazi na idadi ya watu mara baada ya Mkuu wa Mkoa kuhutubia kwenye hafla ya ufungaji  wa mafunzo ya usambazaji na matumizi ya matokeo ya SENSA ya watu na makazi kwa viongozi na makundi mbalimbali kutoka Mkoani Tabora, yaliofanyika katika ukumbi wa Ristalemi, Januari 18, 2024.

Mkuu wa Mkoa amegawa Ramani hizo kwa Watendaji wote wa Kata ishirini na Tisa (29) zilizopo Manispaa ya Tabora.

Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 18, 2023
  • SIKU YA KIMATAIFA YA WANAWAKE MACHI 8 March 07, 2024
  • BEI ELEKEZI YA MBOLEA YA CAN KWA KAMPUNI YA YARA June 15, 2022
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MITAALA YA ELIMU TANZANIA BARA March 23, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • BARAZA LA BIASHARA MKOA WA TABORA LADHAMIRIA KULETA MAGEUZI KATIKA KUBORESHA MAZINGIRA YA BIASHARA NA UWEKEZAJI KWA WANANCHI

    May 21, 2025
  • VIONGOZI WA MIKOA YA TABORA NA KIGOMA WAFANYA KIKAO CHA MAANDALIZI KUELEKEA MAONESHO YA SIKUKUU YA WAKULIMA NANE NANE 2025

    May 20, 2025
  • RC CHACHA AZINDUA MASHINDANO YA UMITASHUMTA NA UMISSETA MKOA WA TABORA, ATOA WITO WA KULINDA NDOTO ZA WATOTO.

    May 19, 2025
  • TABORA YAADHIMISHA SIKU YA KIMATAIFA YA FAMILIA KWA KUTOA WITO WA MALEZI BORA NA KUPINGA UKATILI.

    May 15, 2025
  • Angalia zote

Video

VIJANA WAKAA MEZA MOJA NA RC MKOA WA TABORA
video nyingine

Viungio vya Haraka

  • Maelezo na fomu ya ahadi ya uadilifu kwa watumishi wa umma
  • Guidelines for the use of ICT in government
  • Agriculture
  • MALALAMIKO,PONGEZI NA MAONI INGIA HAPA
  • Bofya hapa Eoffice

Tovuti Muhimu

  • Ikulu
  • Ofisi ya Rais-Tamisemi
  • Ofisi ya Rais-Utumishi
  • SALARYSLIP
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tabora

    S.L.P: 25 Tabora

    Simu: 026 2604058

    Mobile:

    Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa mara
    • Service
    • owner

Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa