• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Nukushi ya malalamiko |
TABORA REGION ADMINISTRATIVE SECRETARY

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi Ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tabora

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Biashara
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo Cha Mawasiliano
    • Muundo
  • Wilaya
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Wilaya ya Urambo
    • Wilaya ya Igunga
    • Wilaya ya Uyui
    • Wilaya ya Kaliua
    • Wilaya ya Sikonge
    • Wilaya ya Nzega
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Tabora
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Halmashauri ya Wilaya ya Igunga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua
    • Halmashauri ya Wilaya Urambo
    • Halmashauri ya Mji wa Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya Sikonge
  • Fursa za Uwekezaji
    • Miombo Project
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi inayoendelea
    • Kilimo
      • Miombo Project
        • Miradi iliyokamilika
        • Miradi inayoendelea
    • Mifugo
    • Opportunity services
    • Viwanda na Biashara
      • New menu item
    • Madini
    • Uvuvi
    • EQUIP-TANZANIA
    • FURSA ZA UWEKEZAJI
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Tafiti
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

SERIKALI NA UNICEF ZAONGEZA JUHUDI KUKUZA USOMAJI WA MASOMO YA SAYANSI KWA WANAFUNZI WA KIKE MKOANI TABORA.

Posted on: March 20th, 2025

Serikali kupitia Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tabora kwa kushirikiana na Shirika la Kuhudumia Watoto Duniani (UNICEF) imezindua mafunzo maalum kwa Maafisa Elimu Sekondari, Maafisa Maendeleo ya Jamii, Waratibu wa UNICEF, na walimu mahili wa masomo ya Sayansi. Mafunzo haya yanafanyika katika ukumbi wa maktaba wa Shule ya Wavulana Tabora, yanalenga kuboresha mbinu za ufundishaji na kuongeza hamasa kwa wanafunzi, hasa wa kike, kusoma masomo ya Sayansi, Teknolojia, Uhandisi na Hisabati (STEM).

Akifungua rasmi mafunzo hayo kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa, Katibu Tawala Msaidizi Miundombinu, Mhandisi Faustine Tarai, alisema kuwa mwitikio wa wanafunzi katika kusoma masomo ya Sayansi bado ni mdogo, hasa kwa somo la Hisabati. Alieleza kuwa tatizo hili linaanzia shule za msingi, ambapo watoto wengi hujenga hofu dhidi ya masomo haya kutokana na ukosefu wa mazingira rafiki ya kujifunza na kutokuwepo kwa hamasa ya kutosha.

Takwimu za mwaka 2024 zinaonyesha kuwa kati ya wanafunzi 15,125 waliomaliza Kidato cha Nne, ni asilimia 24 pekee waliosoma masomo ya Sayansi, ikiwa ni sawa na wanafunzi 3,596. Kati yao, wasichana walikuwa 1,596, hali inayoashiria uwiano mdogo wa wanafunzi wa kike katika masomo ya Sayansi. Hali hii ni sawa pia katika masomo ya Hisabati na Kemia, ambapo idadi ya wanafunzi wa kike bado ni ndogo ukilinganisha na ya wavulana.

Serikali na UNICEF zinahimiza wadau wa elimu kuweka mikakati madhubuti ili kuongeza hamasa kwa wanafunzi, hususan wa kike, kujikita katika masomo ya Sayansi. Mhandisi Tarai alieleza kuwa baadhi ya mbinu zinazopendekezwa ni: Kuboresha upatikanaji wa vifaa vya maabara katika shule za sekondari, Kutoa hamasa kwa walimu na wanafunzi ili kuvunja dhana potofu ya kuwa masomo ya Sayansi ni magumu, Kuhakikisha matumizi sahihi ya rasilimali zilizotolewa kwa ajili ya elimu ya Sayansi, Kuimarisha upangaji wa bajeti kwa ajili ya maendeleo ya elimu ya Sayansi, ikiwemo matumizi ya fedha kutoka serikali kuu pamoja na na mapato ya ndani ya halmashauri.

Kwa upande wao, walimu walioshiriki mafunzo hayo wameipongeza serikali na UNICEF kwa juhudi zao katika kuboresha elimu ya Sayansi nchini, wakiahidi kutumia ujuzi watakaopata kuhamasisha wanafunzi zaidi, hasa wa kike, kupenda masomo ya sayansi.

Akihitimisha hotuba yake, Mhandisi Tarai alisisitiza kuwa dunia ya sasa na inayokuja inahitaji wataalamu wa Sayansi na Teknolojia. Aliitaka jamii nzima kushiriki katika juhudi za kuwahamasisha wanafunzi wa kike kujikita katika masomo ya sayansi ili kuongeza idadi ya wasichana wanaochagua masomo hayo na kupata watalaam wengi wa taaluma za sayansi kwa wakati ujao.

Mafunzo haya, yanayotarajiwa kudumu kwa siku tatu, yanapewa matumaini makubwa ya kuleta mabadiliko chanya katika elimu ya Sayansi nchini.

Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 18, 2023
  • SIKU YA KIMATAIFA YA WANAWAKE MACHI 8 March 07, 2024
  • BEI ELEKEZI YA MBOLEA YA CAN KWA KAMPUNI YA YARA June 15, 2022
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MITAALA YA ELIMU TANZANIA BARA March 23, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • BARAZA LA BIASHARA MKOA WA TABORA LADHAMIRIA KULETA MAGEUZI KATIKA KUBORESHA MAZINGIRA YA BIASHARA NA UWEKEZAJI KWA WANANCHI

    May 21, 2025
  • VIONGOZI WA MIKOA YA TABORA NA KIGOMA WAFANYA KIKAO CHA MAANDALIZI KUELEKEA MAONESHO YA SIKUKUU YA WAKULIMA NANE NANE 2025

    May 20, 2025
  • RC CHACHA AZINDUA MASHINDANO YA UMITASHUMTA NA UMISSETA MKOA WA TABORA, ATOA WITO WA KULINDA NDOTO ZA WATOTO.

    May 19, 2025
  • TABORA YAADHIMISHA SIKU YA KIMATAIFA YA FAMILIA KWA KUTOA WITO WA MALEZI BORA NA KUPINGA UKATILI.

    May 15, 2025
  • Angalia zote

Video

VIJANA WAKAA MEZA MOJA NA RC MKOA WA TABORA
video nyingine

Viungio vya Haraka

  • Maelezo na fomu ya ahadi ya uadilifu kwa watumishi wa umma
  • Guidelines for the use of ICT in government
  • Agriculture
  • MALALAMIKO,PONGEZI NA MAONI INGIA HAPA
  • Bofya hapa Eoffice

Tovuti Muhimu

  • Ikulu
  • Ofisi ya Rais-Tamisemi
  • Ofisi ya Rais-Utumishi
  • SALARYSLIP
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tabora

    S.L.P: 25 Tabora

    Simu: 026 2604058

    Mobile:

    Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa mara
    • Service
    • owner

Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa