Leo Julai 21,2023,, Mkuu wa Wilaya ya Uyui Mhe. Zakaria Mwansasu akimuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian amefungua mfumo wa usafiri wa dharura kwa akina mama wajawazito, waliojifungua na watoto wachanga (M-MAMA) Katika hospitali ya Rufaa ya Kitete iliyopo Manispaa ya Tabora.
Akifungua mfumo huo , Mhe. Mwansasu ameeleza mafanikio makubwa Kwenye Sekta ya Afya yaliofanywa na Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hususani suala la upungufu wa vifo vinavyosababishwa na uzazi kutoka vifo 99 kwa mwaka 2017 hadi vifo 22 kwa mwaka 2023.
“Mheshimiwa Rais amekuwa akituagiza kufanya maboresho zaidi na kuhakikisha kwamba hakuna mwanamke anayefariki kutokana na ujauzito au kujifungua na hakuna mtoto anayefariki kutokana na sababu zinazoweza kuzuilika.”
Sambamba na hilo, Dc Mwansansu ametoa wito kwa wananchi kutumia huduma za afya zinazotolewa na Serikali kwakuwa huduma za afya ya mama na mtoto hutolewa bila malipo.
“Huduma za Afya ya Mama na Mtoto hutolewa bila malipo, na kunafanyika jitihada mbalimbali kuhakikisha huduma bora zinapatikana karibu na wananchi katika Mkoa wetu wa Tabora”
Aidha, Mhe Mwansasu ametoa wito kwa watumishi wa Afya kufanya kazi kwa weledi na maadili ili kutoa huduma bora kwa wananchi. Pia amewapongeza wadau wote wa sekta ya afya kwa mchango wao mkubwa.
Mfumo huu wa M-MAMA ulizinduliwa Dodoma mnamo Aprili 6,2022 na Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Tabora
S.L.P: 25 Tabora
Simu: 026 2604058
Mobile:
Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz
Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa