NA TIGANYA VINCENT
MKOA wa Tabora kwa kushirikiana na Taasisi ya Utafiti wa Kilimo ya Tumbi unatarajia kuendesha zoezi la upimaji wa ubora wa udongo wake ili kuwawezesha wakulima mazao mabalimbali kuzalisha kwa wingi.
Kauli hiyo imetolewa leo na Mkuu wa Mkoa wa Tabora Balozi Dkt. Batilda Buriani wakati wa uzinduzi wa Baraza la Biashara ya Wilaya ya Sikonge.
Alisema zoezi hilo litarajiwa kufanyika katika Halmashauri zote za Mkoa huo katika kiindi cha Mwezi mmoja
Balozi Dkt. Batilda alisema lengo la zoezi hilo ni kutaka kuwahakikisha wakulima kupata mavuno mazuri badala kulima kilimo cha kubahatisha kwa kulima bila kujua kama watafanikiwa.
“Tunataka kufanya ‘soil analysis’ katika Halmashauri zetu zote kwa ajili ya kumwezesha mkulima anapolima ajue anapaswa kulima zao gani katika shamba lake ili aweze kupata mavuno mazuri” alisema.
Alisema wanataka wakulima pindi wanapotaka kulima watambue kuwa ardhi yao inafaa aina fulani ya mazao na kuwaepusha kulima kwa mazoea na kujikuta hawapati faida kubwa.
Balozi Dkt. Batilda alisema kwa kuanzia wameshafanya katika eneo Karangasi wilayani Uyui na kubaini kuwa eneo hilo linafaa sana katika uzalishaji wa alizeti.
Alisema kufuatia hali hiyo wanatarajia kuanzisha mashamba makubwa(block farm) ya alizeti katika eneo ili waweze kuzalisha kwa wingi kwa ajili ya uzalishaji wa mafuta ya kula.
Katika hatua nyingine Mkuu wa Mkoa wa Tabora amekemea vitendo vya uchomaji moto ovyo ambavyo imesababisha uharibifu mkubwa wa mistu katika maeneo mbalimbali ya Wilaya ya Sikonge.
Akizungumza na Wakazi wa Ipole wilayani Sikonge ametaka kuwafichua wanaoendesha vitendo vya uchoamji mistu ovyo ili hatua za kisheria dhidi yao zichukuliwe.
Balozi Dkt. Batilda alisema kuwa viyendo hivyo vinatishia zoezi la ufugaji nyuki ambayo ndio nemboa ya Tabora
Tabora
S.L.P: 25 Tabora
Simu: 026 2604058
Mobile:
Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz
Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa