• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Nukushi ya malalamiko |
TABORA REGION ADMINISTRATIVE SECRETARY

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi Ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tabora

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Biashara
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo Cha Mawasiliano
    • Muundo
  • Wilaya
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Wilaya ya Urambo
    • Wilaya ya Igunga
    • Wilaya ya Uyui
    • Wilaya ya Kaliua
    • Wilaya ya Sikonge
    • Wilaya ya Nzega
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Tabora
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Halmashauri ya Wilaya ya Igunga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua
    • Halmashauri ya Wilaya Urambo
    • Halmashauri ya Mji wa Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya Sikonge
  • Fursa za Uwekezaji
    • Miombo Project
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi inayoendelea
    • Kilimo
      • Miombo Project
        • Miradi iliyokamilika
        • Miradi inayoendelea
    • Mifugo
    • Opportunity services
    • Viwanda na Biashara
      • New menu item
    • Madini
    • Uvuvi
    • EQUIP-TANZANIA
    • FURSA ZA UWEKEZAJI
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Tafiti
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

TABORA YAADHIMISHA SIKU YA KIMATAIFA YA FAMILIA KWA KUTOA WITO WA MALEZI BORA NA KUPINGA UKATILI.

Posted on: May 15th, 2025

Kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Tabora, Katibu Tawala Msaidizi anayeshughulikia Miundombinu, Mhandisi Faustine Mtesigwa Tarai, amefungua Kongamano la Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Familia yaliyofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Mkoa wa Chief Isike Mwanakiyungi, Tabora.

Katika hotuba yake ya ufunguzi wa kongamano hilo, Mhandisi Tarai alisisitiza kuwa familia ni msingi wa jamii na taifa. Alibainisha kuwa changamoto zinazozikumba familia katika nyanja mbalimbali kama ukatili wa kimwili, kingono, kisaikolojia, kiuchumi na kijinsia, zinahitaji juhudi za pamoja kupambana nazo ili kujenga taifa imara.

Mhandisi Tarai alieleza kuwa serikali inaendelea kutekeleza mikakati mbalimbali ya kukabiliana na ukatili wa familia, akitaja miongoni mwa mikakati hiyo kuwa ni utekelezaji wa Mpango wa Taifa wa Kutokomeza Ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto (MTAKUWWA), ambapo vikundi mbalimbali vimeundwa kusaidia kutoa elimu na kuchukua hatua dhidi ya ukatili unaojitokeza.

Kwa upande wake, Afisa Ustawi wa Jamii Mkoa wa Tabora, Ndg. Abakos Kululetela, alieleza kuwa maadhimisho hayo yamelenga kuongeza uelewa kuhusu umuhimu wa familia na kuibua mijadala juu ya changamoto zinazozuia ustawi wa familia, ikiwa ni pamoja na ukatili wa kijinsia na matatizo ya kiuchumi.

Akichangia mjadala , Bi. Agneta John kutoka shirika lisilo la kiserikali la Jikomboe Integral Development Association (JIDA), alieleza kuwa taasisi yao inaendelea kushirikiana kwa karibu na serikali katika kuhakikisha watoto wa Kitanzania wanalelewa katika mazingira bora.

“Tunaamini kuwa namna mtoto anavyolelewa ndicho kiini cha kupata viongozi bora wa kesho. Tukibadili mwanzo wa hadithi ya maisha yao, tunaweza kubadili mustakabali mzima wa familia na taifa,” alisema Bi. Agneta.

Akihitimisha hotuba yake, Mhandisi Tarai alitoa wito kwa jamii kuhakikisha watoto wanapata malezi bora, lishe sahihi, afya njema, pamoja na ulinzi dhidi ya vitendo vya ukatili.

“Tufanye kazi kwa bidii kupunguza umasikini katika familia zetu. Umasikini unachangia ukatili; hali duni ya maisha huwalazimisha watu kuwa wanyonge na kuvumilia ukatili usiostahili,” aliongeza.

Maadhimisho haya yalikusanya wadau mbalimbali wa maendeleo ya familia, ustawi wa jamii, pamoja na mashirika yasiyo ya kiserikali, huku wakiahidi kuendeleza ushirikiano katika kuboresha maisha ya familia za Kitanzania.Kauli mbiu ya maadhimisho haya kwa mwaka 2025 inasema: “Mtoto ni Malezi; Msingi wa Familia Bora kwa Taifa Bora”

Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 18, 2023
  • SIKU YA KIMATAIFA YA WANAWAKE MACHI 8 March 07, 2024
  • BEI ELEKEZI YA MBOLEA YA CAN KWA KAMPUNI YA YARA June 15, 2022
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MITAALA YA ELIMU TANZANIA BARA March 23, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • MHE. CHACHA AIPONGEZA TIMU YA UMISSETA MKOA KWA KUSHIKA NAFASI YA TATU KITAIFA

    July 01, 2025
  • RC. CHA AWAAPISHA WAKUU WA WILAYA WAPYA, WAAHIDI KUFANYA KAZI KWA BIDII NA UADILIFU.

    July 01, 2025
  • TABORA: MASHIRIKA YASIYO YA KISERIKALI YATAKIWA KUZINGATIA SHERIA NA MAADILI YA NCHI

    June 26, 2025
  • MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA YAENDESHA MAFUNZO MAALUM YA MATUMIZI YA MFUMO WA PEPMIS KWA WATUMISHI WA UMMA MKOA WA TABORA

    June 23, 2025
  • Angalia zote

Video

VIJANA WAKAA MEZA MOJA NA RC MKOA WA TABORA
video nyingine

Viungio vya Haraka

  • Maelezo na fomu ya ahadi ya uadilifu kwa watumishi wa umma
  • Guidelines for the use of ICT in government
  • Agriculture
  • MALALAMIKO,PONGEZI NA MAONI INGIA HAPA
  • Bofya hapa Eoffice

Tovuti Muhimu

  • Ikulu
  • Ofisi ya Rais-Tamisemi
  • Ofisi ya Rais-Utumishi
  • SALARYSLIP
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tabora

    S.L.P: 25 Tabora

    Simu: 026 2604058

    Mobile:

    Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa mara
    • Service
    • owner

Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa