Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian amezindua mafunzo ya utengenezaji wa nyuzi na vitambaa kwa kutumia teknolojia kutoka nchi ya Indonesia ambayo yatadumu kwa muda wa siku kumi (10) kuanzia leo Machi 4, 2024 mpaka Machi 14, 2024 katika chuo cha Ufundi VETA kilichopo Manispaa ya Tabora, ambayo yatahusisha baadhi ya vijana wanaojihusisha na shughuri za ushonaji mkoani Tabora.
Akitoa hotuba yake, Mhe. Batilda ametoa shukrani na pongezi kwa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuhimarisha mahusiano ya Tanzania na Indonesia ambayo yamekuwa na tija kwa wakazi wa Tabora, kwa kufaidika na mafunzo hayo ambayo yanakwenda kuleta mabadiliko makubwa katika sekta ya viwanda vidogo vidogo na kuleta ajira kwa vijana.
Naye, Balozi wa Indonesia nchini Tanzania Mhe. Balozi Tri Yogo Jatmiko amesema kuwa, nchi ya Indonesia inatambua jitihadi ya Serikali ya Tanzania katika kuwakwamua vijana kupita mafunzo ya ufundi, na hivyo yeye kama mwakilishi wa taifa hilo ataendelea kutoa ushirikiano kwa Tanzania kuhakikisha fursa mbalimbali zilizopo katika nchi hizo mbili zinakuwa na tija kwa wananchi wa pande zote.
kwa upande mwingine, Mkurugenzi Mkuu wa VETA Dkt. Prosper Mgaya amasema kuwa, licha ya mafunzo hayo kufanyika kwa siku kumi (10) watahakikisha mafunzo hayo yanakuwa endelevu na kuleta tija kwa vijana. Na pia Prof. Mgaya amemuahidi Mkuu wa Mkoa kuendelea kuhimarisha mahusiano kati ya Vyuo vya VETA na ofisi ya Mkuu wa Mkoa ambayo imeonesha nia ya dhati ya kubuni njia mbalimbali za kuwawezesha vijana kupitia mafunzo hayo.
Tabora
S.L.P: 25 Tabora
Simu: 026 2604058
Mobile:
Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz
Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa