Kufuatia ufunguzi wa siku ya Mbolea Duniani ambayo kitaifa yanafanyika Mkoani Tabora, Tume ya Maendeleo ya Ushirika imebainisha mchango wake katika maendeleo ya ushirika ambao unabeba ididi kubwa ya wanachama wanaofaidika na mbolea. Kwa niaba ya Mrajisi na Mtendaji Mkuu wa TCDC, Ndugu. Venance Msafiri Mrajisi Msaidi (M) Tabora ameeleza kuwa, TCDC ina majukumu makubwa mawili ambayo inayatekeleza kupitia vyama vya msingi ambavyo vinajumuhisha idadi kubwa ya wakulima ambao hufaidika na mbolea moja kwa moja.
“tume ina majukumu makubwa mawili, kwanza ni usimamizi na uthibiti wa vyama vyama vya Ushirika na pili ni kufanya uhamsishaji kwenye vyama vya Ushirika na sehemu zote za kiuchumi.” Alisema Mrajisi.
Sambamba na hilo Ndugu, Venance amebainisha umuhimu wa Maadhimisho ya Siku ya Mbolea kwa wakulima ambao mpaka sasa idadi yake ni kubwa na wanafaidika kwa kiasi kikubwa na maadhimisho haya ambayo wakulima wanapata nafasi kubwa ya kujifunza mambo kadha wa kdha kuhusiana na mbolea.
“Nchi nzima kuna vyama vya Ushirika zaidi ya elfu saba na mia tatu (7300) ambavyo vina jumla ya wanachama milioni nane (8,000,000), na kati ya hao AMCOS ina wanachama 5000 ambao kwenye maadhimisho haya, ile idadi kubwa ya wanachama kuna idadi kubwa ya wakulima na wanatumia hizi mbolea” Alisisitiza Ndugu Msafiri.
Aidha, Ndugu Venance Msafiri ameeleza kuwa, maadhimisho haya ya Siku ya Mbolea yana faida kubwa kwa wakulima Mkoani Tabora kwani kuna idadi kubwa ya wakulima ambao hufaidika moja kwa moja na mbolea zinazotolewa.
“Kwa mfano sisi hapa Tabora tunatumia mbolea aina mbalimbali na tunashukuru sana kwa mwaka huu bei ya mbolea imeshuka chini na kumuwezesha mkulima kumudu bei hiyo”alisema ndugu Venance.
Ikumbukwe kuwa, Maadhimisho ya Siku ya Mbolea Duniani yanafanyika Mkoani Tabora kuanzia Oktoba 11, 2023 hadi Oktoba 13, 2023, yenye Kauli mbiu isemayo “Matumizi Sahihi ya Mbolea ya Ruzuku kwa Kilimo Chenye Tija”
Tabora
S.L.P: 25 Tabora
Simu: 026 2604058
Mobile:
Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz
Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa