Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batlida Salha Buriani ameupongeza ugeni wa watu 10 kutoka nchini Afrika Kusini uliokuja kujifunza kuhusu ufugaji nyuki huku akisema ujio wao utasaidia kumarisha biashara ya ufugaji nyuki baina ya Tanzania na nchi hiyo.
Akizungumza katika hafla ya kuwaaga wageni hao iliyofanyika leo Julai 28, 2023 kwenye ukumbi wa Isike Mwanakiyungi Mkoani Tabora, Balozi Dkt. Burian amesema, ugeni huo una faida kwa Tanzania kwani utachochea mahusiano mazuri kwenye eneo la ufugaji nyuki pamoja na kuitangaza asali ya Tanzania Kimataifa kwani wamevutiwa ubora wa asali hiyo.
"Tanzania na Afrika Kusini ni ndugu na Sisi tutaendelea kuimarisha mahusiano yaliyojengwa na Waasisi wetu wa nchi hizi mbili kwa kuhakikisha ufugaji wa nyuki unakuwa endelevu kwetu sote "amesema Dkt. Batilda
Aidha, amesema Mkoa wa Tabora umefarijika na ugeni huo ambao utawawezesha wafugaji nyuki kunufaika na masoko ya kimataifa.
"Namshukuru Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuendelea kuifungua Tanzania kimataifa na hi kwetu Tabora ni fursa ya kunadi asali yetu ." ameongeza.
Mnamo Julai 26, 2023 Mkoa wa Tabora ulipokea Wageni kumi (10) kutoka nchi ya Afrika Kusini ambao walikuwa na Ziara ya Siku tatu Mkoani hapa kwa lengo la kujifunza masuala mbalimbali ya Ufugaji wa Nyuki. Na wageni hao wanatarajia kuondoka Mkoani Tabora Julai 29, 2023.
Tabora
S.L.P: 25 Tabora
Simu: 026 2604058
Mobile:
Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz
Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa