• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Nukushi ya malalamiko |
TABORA REGION ADMINISTRATIVE SECRETARY

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi Ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tabora

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Biashara
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo Cha Mawasiliano
    • Muundo
  • Wilaya
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Wilaya ya Urambo
    • Wilaya ya Igunga
    • Wilaya ya Uyui
    • Wilaya ya Kaliua
    • Wilaya ya Sikonge
    • Wilaya ya Nzega
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Tabora
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Halmashauri ya Wilaya ya Igunga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua
    • Halmashauri ya Wilaya Urambo
    • Halmashauri ya Mji wa Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya Sikonge
  • Fursa za Uwekezaji
    • Miombo Project
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi inayoendelea
    • Kilimo
      • Miombo Project
        • Miradi iliyokamilika
        • Miradi inayoendelea
    • Mifugo
    • Opportunity services
    • Viwanda na Biashara
      • New menu item
    • Madini
    • Uvuvi
    • EQUIP-TANZANIA
    • FURSA ZA UWEKEZAJI
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Tafiti
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

VIONGOZI WA MIKOA YA TABORA NA KIGOMA WAFANYA KIKAO CHA MAANDALIZI KUELEKEA MAONESHO YA SIKUKUU YA WAKULIMA NANE NANE 2025

Posted on: May 20th, 2025

Mkuu wa Wilaya ya Sikonge, Mhe. Cornel Lucas Magembe, kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Mhe. Paulo Chacha, ameongoza kikao cha maandalizi ya maonesho ya wakulima – Nanenane 2025, kilichofanyika katika ukumbi wa Chief Isike Mwanakiyungi, Manispaa ya Tabora.

Kikao hicho kilihusisha viongozi pamoja na wataalamu ngazi za wilaya na mikoa kutoka mikoa  ya Tabora na Kigoma,lengo ni kuweka mikakati thabiti ya kuboresha maandalizi ya maonesho ya sikukuu ya wakulima – nane nane  2025.

Akizungumza katika kikao hicho, Katibu Tawala Msaidizi anayeshughulikia Uchumi na Uzalishaji Mkoa wa Tabora, Bw. Abraham Mndeme, aliwasilisha tathmini ya maonesho ya mwaka 2024 na kubainisha kuwa Manispaa ya Kigoma iliibuka mshindi wa kwanza kati ya washiriki wote wa kanda ya magharibi.

Katika kikao hicho, wajumbe waliagizwa kuwajulisha Wakurugenzi Watendaji wa halmashauri zote za Tabora na Kigoma kuanza mapema maandalizi ya maonesho hayo, ikiwa ni pamoja na kuandaa mpango kazi mahsusi wa maonesho ili kuwavutia wawekezaji zaidi. Wadau pia walihimizwa kuwaelimisha wakulima, wafugaji na wavuvi kuhusu matumizi ya teknolojia za kisasa ili kuongeza tija na ubora katika uzalishaji

.

Akihitimisha kikao hicho, Mhe. Magembe alibainisha maazimio kadhaa yaliyopitishwa na wajumbe, likiwemo pendekezo la wadau wa maonesho kuchangia vitu halisi badala ya fedha, ili kurahisisha utekelezaji wa shughuli kwa wakati.

“Tumegundua kuwa michango ya kifedha huchukua muda mrefu kufanikishwa kutokana na taratibu za kifedha. Kwa kuchangia vifaa na huduma moja kwa moja, tutaokoa muda na kuongeza ufanisi,” alisema Mhe. Magembe.

Aidha, upatikanaji wa huduma ya maji ya uhakika katika eneo la maonesho umetajwa kuwa kipaumbele ili kuwezesha maandalizi ya vitalu vya maonesho kwa ufanisi.

Mhe. Magembe aliwashukuru wajumbe kwa michango yao, akisema kuwa maazimio ya kikao hicho yatasaidia kuboresha kwa kiwango kikubwa maonesho ya mwaka huu.

Maonesho ya Nanenane kwa kanda ya Magharibi yanatarajiwa kufanyika katika viwanja vya Ipuli, Manispaa ya Tabora, yakijumuisha mikoa ya Tabora na Kigoma, huku maadhimisho ya kitaifa yakifanyika jijini Dodoma.

Kaulimbiu ya mwaka huu ni: "Chagua Viongozi Bora kwa Maendeleo Endelevu ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi 2025."

Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 18, 2023
  • SIKU YA KIMATAIFA YA WANAWAKE MACHI 8 March 07, 2024
  • BEI ELEKEZI YA MBOLEA YA CAN KWA KAMPUNI YA YARA June 15, 2022
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MITAALA YA ELIMU TANZANIA BARA March 23, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • MHE. CHACHA AIPONGEZA TIMU YA UMISSETA MKOA KWA KUSHIKA NAFASI YA TATU KITAIFA

    July 01, 2025
  • RC. CHA AWAAPISHA WAKUU WA WILAYA WAPYA, WAAHIDI KUFANYA KAZI KWA BIDII NA UADILIFU.

    July 01, 2025
  • TABORA: MASHIRIKA YASIYO YA KISERIKALI YATAKIWA KUZINGATIA SHERIA NA MAADILI YA NCHI

    June 26, 2025
  • MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA YAENDESHA MAFUNZO MAALUM YA MATUMIZI YA MFUMO WA PEPMIS KWA WATUMISHI WA UMMA MKOA WA TABORA

    June 23, 2025
  • Angalia zote

Video

VIJANA WAKAA MEZA MOJA NA RC MKOA WA TABORA
video nyingine

Viungio vya Haraka

  • Maelezo na fomu ya ahadi ya uadilifu kwa watumishi wa umma
  • Guidelines for the use of ICT in government
  • Agriculture
  • MALALAMIKO,PONGEZI NA MAONI INGIA HAPA
  • Bofya hapa Eoffice

Tovuti Muhimu

  • Ikulu
  • Ofisi ya Rais-Tamisemi
  • Ofisi ya Rais-Utumishi
  • SALARYSLIP
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tabora

    S.L.P: 25 Tabora

    Simu: 026 2604058

    Mobile:

    Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa mara
    • Service
    • owner

Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa