Mkuu wa Mkoa amengoza kuwa, licha ya idadi hiyo ya wananchi kukabidhiwa vitambulisho hivyo, bado wananchi zaidi ya laki moja hawajakabidhiwa vitambulisho vyao, na hivyo kutoa wito kwa wananchi kuwa na subira wakati zoezi la uandikishwaji likiendelea.
Sambamba na hilo Mhe. Batilda amemshukuru Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuendelea kutoa fedha na kukamilsha zoezi hili la utolewaji wa vitambulisho vya taifa ambalo kwa mkoa wa Tabora limefanikiwa kwa kiasi kikubwa sana.
Aidha Mhe. Burian ametoa wito kwa wakuu wa wilaya na wakurugenzi kuhakikisha wanasimamia zoezi hili la ugawaji wa vitambulisho vya taifa kwenye halmashauri zote za mkoa wa Tabora.
Kwa upande wa Afisa usajili wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa Mkoa wa Tabora Ndugu. Isakwisa Mwampulo amebainisha baadhi ya changamoto ambazo bado zipo kwenye ukamilishaji wa zoezi hilo ikiwemo, tabia ya wananchi kutoa taarifa za uongo na na masuala ya uraia, na kuahidi kuzidi kufanya kazi kwa bidii ili kukamilisha zoezi hilo kwa kushirikiana na watendaji wa kata na vijiji.
Nao baadhi ya wananchi wametoa shukrani kwa kupata vitambulisho hivyo ambavyo vimekuwa na msaada mkubwa sana, na kwamba hapo awali walikuwa wakikosa baadhi ya huduma muhimu kwa kukosekana kwa baadhi ya taarifa muhimu zilizopo kwenye vitambulisho hivyo.
Tabora
S.L.P: 25 Tabora
Simu: 026 2604058
Mobile:
Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz
Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa