• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Nukushi ya malalamiko |
TABORA REGION ADMINISTRATIVE SECRETARY

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi Ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tabora

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Biashara
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo Cha Mawasiliano
      • Community development
    • Muundo
  • Wilaya
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Wilaya ya Urambo
    • Wilaya ya Igunga
    • Wilaya ya Uyui
    • Wilaya ya Kaliua
    • Wilaya ya Sikonge
    • Wilaya ya Nzega
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Tabora
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Halmashauri ya Wilaya ya Igunga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua
    • Halmashauri ya Wilaya Urambo
    • Halmashauri ya Mji wa Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya Sikonge
  • Fursa za Uwekezaji
    • Miombo Project
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi inayoendelea
    • Kilimo
      • Miombo Project
        • Miradi iliyokamilika
        • Miradi inayoendelea
    • Mifugo
    • Opportunity services
    • Viwanda na Biashara
      • New menu item
    • Madini
    • Uvuvi
    • EQUIP-TANZANIA
    • FURSA ZA UWEKEZAJI
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Tafiti
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

WASHIRIKI WA KOZI YA 14 CHUO CHA ULINZI WA TAIFA WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO KWA VITENDO MKOANI TABORA

Posted on: January 15th, 2026

Washiriki wa Kozi ya 14 kutoka Chuo cha Taifa cha Ulinzi (NDC), wakitoka katika mataifa saba ambayo ni Misri, Malawi, Rwanda, Burundi, Kenya, India na Tanzania, wamewasili mkoani Tabora kwa ziara ya mafunzo kwa vitendo itakayodumu kwa muda wa siku sita, ikiwa na lengo la kujifunza na kujionea utekelezaji wa shughuli mbalimbali katika nyanja za siasa, uchumi na maendeleo ya kijamii.


Ziara hiyo mkoani Tabora inaongozwa na Kaimu Mkuu wa Chuo cha Taifa cha Ulinzi, Brigedia Jenerali Charles Ndiege, ambapo wamepokelewa rasmi na Mkuu wa Wilaya ya Kaliua, Mhe. Dkt. Gelard Mongella, kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Tabora.


Katika kipindi cha ziara yao, washiriki wa mafunzo hayo wanatarajia kutembelea na kujionea miradi na taasisi mbalimbali za kimkakati ikiwemo Kiwanda cha kutengeneza mkaa mbadala cha Kuja na Kushoka kilichopo Manispaa ya Tabora, Ranchi ya kisasa ya ng’ombe wa maziwa wilayani Uyui, pamoja na mradi wa ujenzi wa bomba la mafuta ghafi katika eneo la Sojo.


Aidha, kundi hilo pia linatarajia kutembelea Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI) – Tumbi, pamoja na Kiwanda cha kuchakata mazao ya nyuki kilichopo wilayani Sikonge, ili kupata uelewa wa moja kwa moja kuhusu jitihada za Serikali katika kuimarisha uzalishaji na kukuza uchumi wa viwanda.


Ziara hiyo ni sehemu ya mafunzo ya vitendo kwa washiriki wa Kozi ya 14 ya Chuo cha Taifa cha Ulinzi, yenye lengo la kuwajengea uelewa wa kina kuhusu uhalisia wa utekelezaji wa sera na mipango ya maendeleo ya Serikali katika mikoa ya Mwanza, Geita, Singida, Kilimanjaro, Tanga, Njombe, Iringa na Tabora.


Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 18, 2023
  • SIKU YA KIMATAIFA YA WANAWAKE MACHI 8 March 07, 2024
  • BEI ELEKEZI YA MBOLEA YA CAN KWA KAMPUNI YA YARA June 15, 2022
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MITAALA YA ELIMU TANZANIA BARA March 23, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • WASHIRIKI KUTOKA CHUO CHA TAIFA CHA ULINZI - TANZANIA WAHITIMISHA ZIARA YAO MKOANI TABORA KWA KUTEMBELEA KIWANDA CHA KUCHAKATA MAZAO YA NYUKI SIKONGE

    January 17, 2026
  • WASHIRIKI WA KOZI YA 14 CHUO CHA ULINZI WA TAIFA WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO KWA VITENDO MKOANI TABORA

    January 15, 2026
  • MZAZI / MLEZI! SHULE ZIMEFUNGULIWA LEO! MPELEKE MTOTO SHULE. ELIMU NI BURE!.

    January 13, 2026
  • MHE. KAMANI ATATUA KERO ZA WAFUGAJI MKOA WA TABORA, AAGIZA WATAALAM KUSHUKA UWANDANI KUWAHUDUMIA WANANCHI

    January 08, 2026
  • Angalia zote

Video

VIJANA WAKAA MEZA MOJA NA RC MKOA WA TABORA
video nyingine

Viungio vya Haraka

  • Maelezo na fomu ya ahadi ya uadilifu kwa watumishi wa umma
  • Guidelines for the use of ICT in government
  • Agriculture
  • MALALAMIKO,PONGEZI NA MAONI INGIA HAPA
  • Bofya hapa Eoffice
  • Migration Tanzania

Tovuti Muhimu

  • Ikulu
  • Ofisi ya Rais-Tamisemi
  • Ofisi ya Rais-Utumishi
  • SALARYSLIP
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tabora

    S.L.P: 25 Tabora

    Simu: 026 2604058

    Mobile:

    Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa mara
    • Service
    • owner

Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa