• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Nukushi ya malalamiko |
TABORA REGION ADMINISTRATIVE SECRETARY

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi Ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tabora

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Biashara
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo Cha Mawasiliano
    • Muundo
  • Wilaya
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Wilaya ya Urambo
    • Wilaya ya Igunga
    • Wilaya ya Uyui
    • Wilaya ya Kaliua
    • Wilaya ya Sikonge
    • Wilaya ya Nzega
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Tabora
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Halmashauri ya Wilaya ya Igunga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua
    • Halmashauri ya Wilaya Urambo
    • Halmashauri ya Mji wa Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya Sikonge
  • Fursa za Uwekezaji
    • Miombo Project
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi inayoendelea
    • Kilimo
      • Miombo Project
        • Miradi iliyokamilika
        • Miradi inayoendelea
    • Mifugo
    • Opportunity services
    • Viwanda na Biashara
      • New menu item
    • Madini
    • Uvuvi
    • EQUIP-TANZANIA
    • FURSA ZA UWEKEZAJI
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Tafiti
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

WASOMI NCHINI KUANDIKA HISTORIA UPYA HISTORIA YA UKOMBOZI WA TANZANIA

Posted on: March 15th, 2019

WASOMI NCHINI KUANDIKA HISTORIA UPYA HISTORIA YA UKOMBOZI WA TANZANIA

WASOMI wa Kitanzania kutoka  Vyuo Vikuu wametakiwa kuandika historia ya Watanzania mbalimbali waliotoa mchango mkubwa katika kupinga ukoloni nchini ili vijana waweze kupata picha halisi ya harakati za mapambani dhidi ya wakoloni.

Kauli hiyo imetolewa leo wilayani Urambo na Waziri wa Habari, Utamaduni , Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe wakati wa ziara ya kikazi ya kutembelea maeneo ya urithi wa historia ya ukombozi wa Bara la Afrika.

Alisema waandishi wengi waliondika historia ya Tanzania ikiwemo mapambano dhidi ya ukoloni walitoka nje ya nchi na kuandika kwa matakwa yao na hivyo kuacha baadhi ya mashujaa wengi waliopinga kutawaliwa na wakoloni bila kuandikwa.

Dkt. Mwakyembe alisema katika mikoa mbalimbali imebainika kuwepo kwa watu walitoa upinzani mkali kwa Wajerumani na Waingereza lakini hakuna sehemu wanapotajwa katika vitabu wa historia za nchi ya Tanzania.

“Kuna mama Liti kutoka Singida alipambana na Wajerumani kwa kutumia nyuki lakini hakuna vitabu wa historia vinavyomzungumzia…kuna mama mmoja Manyoni ambaye yupo hai hadi leo alimuokoa Mwalimu Nyerere asikamatwe na Waingereza baada ya kumvalisha baibui na kisha kuungana naye lakini hakuna alipoandikwa” alisema.

“Mtemi Isike ni miongoni wa viongozi waliotoa upinzani mkubwa kwa Wajerumani na baadae akajipiga risasi kwa kukataa kukamatwa na Wajerumani , lakini hakuna vitabu vya historia vinapoeleza…tuna utajiri wa historia kubwa lakini iliyosndikwa ni sehemu kidogo sana” aliongeza.

Alisema hatua hiyo imesababisha vijana wengi kutokuwa na historia kubwa ya wapigania uhuru hapa nchini.

Dkt.Mwakyembe alisema wakati umefika wa Wasomi na wataalamu waliopo katika Vyuo vikuu mbalimbali hapa nchini kukaa chini na kufanya utafiti na kuandika historia ya urithi wa ukombozi hapa nchini kwa ajili ya kizazi cha sasa na kijacho.

Mmoja wa Wazee wa Urambo John Samwel alisema Serikali imefanya vizuri kuanza kuyatambua maeneo ya urithi wa kihistoria ya ukumbozi kwa ajili ya kuandika historia ya pana ya mapambano dhidi ya ukoloni nchini Tanzania.

Alisema hatua hiyo itasaidia kuondoa upotoshaji uliofanywa na waandishi kutoka mataifa ya nje ya bara la Afrika ikiwemo kudai uvumbuzi wa Ziwa Victoria , Mlima Kilimanjaro kugunduliwa na wazungu wakati walikuwepo Watanzania wenyeji wa maeneo hayo.

Samwel alisema ni vema historia iandike ukweli ili kuepuka kuwapotosha vijana na vizazi vijavyo.

 

Mwisho

Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 18, 2023
  • SIKU YA KIMATAIFA YA WANAWAKE MACHI 8 March 07, 2024
  • BEI ELEKEZI YA MBOLEA YA CAN KWA KAMPUNI YA YARA June 15, 2022
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MITAALA YA ELIMU TANZANIA BARA March 23, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • MHE. CHACHA AIPONGEZA TIMU YA UMISSETA MKOA KWA KUSHIKA NAFASI YA TATU KITAIFA

    July 01, 2025
  • RC. CHA AWAAPISHA WAKUU WA WILAYA WAPYA, WAAHIDI KUFANYA KAZI KWA BIDII NA UADILIFU.

    July 01, 2025
  • TABORA: MASHIRIKA YASIYO YA KISERIKALI YATAKIWA KUZINGATIA SHERIA NA MAADILI YA NCHI

    June 26, 2025
  • MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA YAENDESHA MAFUNZO MAALUM YA MATUMIZI YA MFUMO WA PEPMIS KWA WATUMISHI WA UMMA MKOA WA TABORA

    June 23, 2025
  • Angalia zote

Video

VIJANA WAKAA MEZA MOJA NA RC MKOA WA TABORA
video nyingine

Viungio vya Haraka

  • Maelezo na fomu ya ahadi ya uadilifu kwa watumishi wa umma
  • Guidelines for the use of ICT in government
  • Agriculture
  • MALALAMIKO,PONGEZI NA MAONI INGIA HAPA
  • Bofya hapa Eoffice

Tovuti Muhimu

  • Ikulu
  • Ofisi ya Rais-Tamisemi
  • Ofisi ya Rais-Utumishi
  • SALARYSLIP
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tabora

    S.L.P: 25 Tabora

    Simu: 026 2604058

    Mobile:

    Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa mara
    • Service
    • owner

Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa