WATU watatu wa Kijiji cha Misheni wilayani Sikonge wamefariki duniani baada ya kuangukiwa na kifusi wakati wakichimba molamu.
Taarifa hiyo imetolewa na Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Tabora ACP Richard Abwao wakati wa mkutano na waandishi wa habari Ofisini kwake,
Alisema chanzo kilichosababisha vifo hivyo ni pamoja na kuporomoka kwa udongo na kuwaangukia marehemu wakati wakiwa chini wakichimba molamu.
Aliwataja waliofariki kuwa ni Bakari Shaban, Sadiki Ramadhan na Rashid Hamisi.
Wakati huo ACP Abwao alisema Jeshi la Polisi linaendelea na misako na doria katika maeneo mbalimbali ambapo limefanikiwa kupata silaha aina ya Pistol iliyotengenezwa kienyeji iliyokuwa ikutumiwa na Vijana kuendesha vitendo vya kiharifu maeneo mbalimbali.
Alisema silaha hiyo ilipatikana katika Pagale (jengo bovu) ambalo lilikuwa likitumiwa na baadhi ya Vijana katika Kata ya Kiloleni kuendesha vitendo vya kiharifu ikiwemo kuwatishia watu na kuwapora mali zao.
Kamanda huyo alisema baada ya Vijana walikuwemo katika Pagale hilo kuwaona Polisi walikimbia na kuacha silaha hiyo.
ACP Abwao aliwasisitiza wananchi wa Mkoa wa Tabora ambao wanamiliki silaha kinyume cha Sheria kuendelea kuzisalimisha kabla ya kipindi cha msamaha ambacho kitakoma mwishoni mwa mwezi huu.
Aliwataka hao kuhakikisha wanapeleka silaha hizo katika Vituo vya Polisi, Ofisi za Kata na zile za Serikali za Mitaa na kuongeza watakaokaidi watachukuliwa hatua.
Tabora
S.L.P: 25 Tabora
Simu: 026 2604058
Mobile:
Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz
Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa