Waziri wa Kilimo Mhe. Hussein Bashe amesema kuwa Serikali ina mpango wa kuhakikisha Mkoa wa Tabora unakuwa kituo kikuu cha Ushirika hapa nchini. Ameyasema hayo leo Julai 1, 2023 wakati akihutubia mamia ya wananchi katika viwanja vya Nanenane,Manispaa ya Tabora kwenye Ufungaji wa Maadhimisho ya Siku ya Ushirika Duniani (SUD). Na kwamba Serikali kwa kushirikiana na wadau wa sekta ya Kilimo watahakikisha wanaufanya Mkoa wa Tabora kuwa kituo cha Ushirika licha ya kwamba Siku ya Ushirika huadhimishwa kwenye mikoa tofautitofauti.
Kwa upande mwingine Waziri Bashe amebainisha kuwa “ hadi sasa jumla ya Kilo milioni 104 zenye thamani ya zaidi ya Shilingi Bilioni 500 za tumbaku zimenunuliwa hadi sasa katika.masoko ya tumbaku yanayoendelea sehemu mbalimbali nchini. Ambapo kilo zilizonunuliwa ni sawa na asilimia 86.6 ya tumbaku ambayo Serikalo kwa mwaka huu imelengwa kununuliwa msimu huu ambayo ni sawa na kilio Milioni 120.
Akifunga maadhimisho ya siku ya ushirika Duniani,SUD,yanayofanyika Kitaifa mkoani Tabora,Julai 1,2023,Waziri wa Kilimo,Hussein Bashe,amesema ana uhakika lengo litafikiwa la kununuliwa kilo 120milioni. Amebainisha kuwa kati ya tumbaku iliyonunuliwa yenye thamani ya zaidi ya Shilingi Bilioni 500 makampuni yamelipa Shilingi Bilioni 400 na yanadaiwa jumla ya Shilingi Bilioni 100..
Ameeleza kuwa msimu uliopita wakulima waliuza kilo Milioni 60 na kwamba waliweka makubaliano ya kufikia kilo 120milioni msimu huu ambazo zitafikiwa."Tumekuwa na ongezeko hilo na nina amini tutalifikia masoko yatakapofikia mwisho msimu huu,"amesema Waziri Hussein Bashe.
Maadhimisho ya Siku ya Ushirika Duniani yalifunguliwa Juni 27,2023 na Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. David Silinde(MB) na kufungwa leo Julai 1, 2023 na Waziri wa Kilimo Mhe. Hussein Bashe(MB).
Kauli mbiu inasema:
“USHIRIKA KWA MAENDELEO ENDELEVU”
Tabora
S.L.P: 25 Tabora
Simu: 026 2604058
Mobile:
Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz
Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa