Leo Julai 21, Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Salha Burian akiambatana na baadhi ya Viongozi wa CCM, viongozi wa dini, baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Usalama ya Mkoa na wakuu wa taasisi za Serikali , wametembelea ofisi za kituo cha Redio cha UYUI FM na kujionea shughuli mbalimbali za urushwaji wa matangazo kupitia masafa ya Fm 99.3
Katika ziara hiyo Mhe. Batilda Burian alifanikiwa kujionea shughuli mbalimbali zinazofanywa na kituo hiko cha matangazo cha UYUI FM na ameupongeza uongozi mzima wa kituo hiko kwa machango wao mkubwa wa utoaji wa habari kwa Wananchi na ushiriki wao katika shughuli mbalimbali za Serikali.
Tabora
S.L.P: 25 Tabora
Simu: 026 2604058
Mobile:
Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz
Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa