• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Nukushi ya malalamiko |
TABORA REGION ADMINISTRATIVE SECRETARY

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi Ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tabora

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Biashara
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo Cha Mawasiliano
    • Muundo
  • Wilaya
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Wilaya ya Urambo
    • Wilaya ya Igunga
    • Wilaya ya Uyui
    • Wilaya ya Kaliua
    • Wilaya ya Sikonge
    • Wilaya ya Nzega
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Tabora
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Halmashauri ya Wilaya ya Igunga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua
    • Halmashauri ya Wilaya Urambo
    • Halmashauri ya Mji wa Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya Sikonge
  • Fursa za Uwekezaji
    • Miombo Project
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi inayoendelea
    • Kilimo
      • Miombo Project
        • Miradi iliyokamilika
        • Miradi inayoendelea
    • Mifugo
    • Opportunity services
    • Viwanda na Biashara
      • New menu item
    • Madini
    • Uvuvi
    • EQUIP-TANZANIA
    • FURSA ZA UWEKEZAJI
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Tafiti
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

BARAZA LA BIASHARA MKOA WA TABORA LADHAMIRIA KULETA MAGEUZI KATIKA KUBORESHA MAZINGIRA YA BIASHARA NA UWEKEZAJI KWA WANANCHI

Posted on: May 21st, 2025

Katika hatua ya kuimarisha mazingira ya biashara na kuchochea ustawi wauchumi wa wananchi, Mkuu wa Wilaya ya Sikonge, Mhe. Cornel Lucas Magembe,ameongoza kikao cha Baraza la Biashara Mkoa wa Tabora kwa niaba ya Mkuu waMkoa, Mhe. Paul Chacha. Kikao hicho kimefanyika katika ukumbi mdogo wa ofisi yaMkuu wa Mkoa wa Tabora, kikiwakutanisha wadau kutoka sekta binafsi na za ummakujadili masuala muhimu ya maendeleo ya biashara mkoani humo.

 

Akifungua kikao hicho, Mhe. Magembe ametoa witokwa Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi wa Halmashauri kuhakikisha wanawawezeshawananchi kuandaa maandiko ya miradi na kuyawasilisha kwenye mifuko na programumbalimbali chini ya Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC). Piaamesisitiza kuimarishwa kwa Majukwaa ya Uwezeshaji Wanawake Kiuchumi hadi ngaziya kata, kutengwa kwa maeneo ya machinga na kuwezeshwa kwa miundombinu rafiki,pamoja na kuhamasisha sekta binafsi kushiriki kikamilifu katika shughuli zamabaraza ya biashara ili kuinua uchumi wa wilaya husika.

“Kila wilaya inapaswa kuwa na mpango mkakati wa kuimarisha ushirikiano katiya serikali na sekta binafsi. Hili ni jambo la msingi katika kujenga uchumishirikishi na endelevu,” alisema Mhe. Magembe.

 

Wadau mbalimbali walioshiriki baraza hilowalitumia fursa hiyo kuibua changamoto zinazokwamisha ustawi wa biashara, ikiwani pamoja na ukosefu wa uhusiano mzuri kati ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA)na wafanyabiashara, mazingira duni ya kufanyia biashara, pamoja na sheriazisizoakisi hali halisi ya wajasiriamali waliowengi.

 

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Chemba yaBiashara, Viwanda na Kilimo Tanzania (TCCIA) Mkoa wa Tabora, Bw. KassongoMirambo, alitoa wito kwa waandaaji wa vikao vya baraza kuhakikisha kuwa wajumbewanapewa mwaliko na nyaraka za kikao mapema ili kuwapa muda wa kujiandaaipasavyo. Alisisitiza umuhimu wa mjadala wa kina unaojikita katika mustakabaliwa biashara na viwanda vya mkoa huo.

 

Naye Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Tabora, Bw. Asanterabi Sang’enoi,aliahidi kuwa serikali ya mkoa itafanyia kazi maoni na mapendekezo yoteyaliyowasilishwa na wajumbe wa baraza hilo. Alisema kuwa serikali inalengakuhakikisha kuwa vikao vya baraza vinafanyika kwa wakati katika mamlaka zote zaserikali za mitaa na kuondoa vikwazo vinavyokwamisha ustawi wa wafanyabiashara.

 

“Fursa zipo nyingi. Serikali imedhamiria kwadhati kuondoa vikwazo vyote vinavyosababisha usumbufu kwa wafanyabiashara ilikuchochea ukuaji wa uchumi wa taifa,” alibainisha Bw. Sang’enoi.

 

Baraza la Biashara Mkoa wa Tabora ni chombohalali kisheria kinachokutana angalau mara moja kwa mwaka kwa lengo la kujadilichangamoto zinazoikabili sekta ya biashara na kuweka mikakati ya kuzitatua,hatua inayolenga kuboresha mazingira ya biashara na kuinua uchumi wa wananchi.

Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 18, 2023
  • SIKU YA KIMATAIFA YA WANAWAKE MACHI 8 March 07, 2024
  • BEI ELEKEZI YA MBOLEA YA CAN KWA KAMPUNI YA YARA June 15, 2022
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MITAALA YA ELIMU TANZANIA BARA March 23, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • BARAZA LA BIASHARA MKOA WA TABORA LADHAMIRIA KULETA MAGEUZI KATIKA KUBORESHA MAZINGIRA YA BIASHARA NA UWEKEZAJI KWA WANANCHI

    May 21, 2025
  • VIONGOZI WA MIKOA YA TABORA NA KIGOMA WAFANYA KIKAO CHA MAANDALIZI KUELEKEA MAONESHO YA SIKUKUU YA WAKULIMA NANE NANE 2025

    May 20, 2025
  • RC CHACHA AZINDUA MASHINDANO YA UMITASHUMTA NA UMISSETA MKOA WA TABORA, ATOA WITO WA KULINDA NDOTO ZA WATOTO.

    May 19, 2025
  • TABORA YAADHIMISHA SIKU YA KIMATAIFA YA FAMILIA KWA KUTOA WITO WA MALEZI BORA NA KUPINGA UKATILI.

    May 15, 2025
  • Angalia zote

Video

VIJANA WAKAA MEZA MOJA NA RC MKOA WA TABORA
video nyingine

Viungio vya Haraka

  • Maelezo na fomu ya ahadi ya uadilifu kwa watumishi wa umma
  • Guidelines for the use of ICT in government
  • Agriculture
  • MALALAMIKO,PONGEZI NA MAONI INGIA HAPA
  • Bofya hapa Eoffice

Tovuti Muhimu

  • Ikulu
  • Ofisi ya Rais-Tamisemi
  • Ofisi ya Rais-Utumishi
  • SALARYSLIP
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tabora

    S.L.P: 25 Tabora

    Simu: 026 2604058

    Mobile:

    Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa mara
    • Service
    • owner

Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa