• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Nukushi ya malalamiko |
TABORA REGION ADMINISTRATIVE SECRETARY

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi Ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tabora

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Biashara
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo Cha Mawasiliano
    • Muundo
  • Wilaya
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Wilaya ya Urambo
    • Wilaya ya Igunga
    • Wilaya ya Uyui
    • Wilaya ya Kaliua
    • Wilaya ya Sikonge
    • Wilaya ya Nzega
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Tabora
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Halmashauri ya Wilaya ya Igunga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua
    • Halmashauri ya Wilaya Urambo
    • Halmashauri ya Mji wa Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya Sikonge
  • Fursa za Uwekezaji
    • Miombo Project
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi inayoendelea
    • Kilimo
      • Miombo Project
        • Miradi iliyokamilika
        • Miradi inayoendelea
    • Mifugo
    • Opportunity services
    • Viwanda na Biashara
      • New menu item
    • Madini
    • Uvuvi
    • EQUIP-TANZANIA
    • FURSA ZA UWEKEZAJI
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Tafiti
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

BODI YA WADHAMINI MFUKO WA MISITU TANZANIA YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO TABORA.

Posted on: May 7th, 2025

Mkuu wa Wilaya ya Nzega, Mhe. Naitapwaki Lemei Tukai, kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Mhe. Paulo Chacha, amewapokea rasmi wajumbe wa Bodi ya Wadhamini wa Mfuko wa Misitu Tanzania waliowasili mkoani humo kwa ziara ya kikazi. Ujumbe huo umeongozwa na Mwenyekiti wa Bodi, Prof. Shabani Chamshama, ambapo lengo la ziara hiyo ni kukagua na kujionea maendeleo ya miradi inayofadhiliwa na mfuko huo katika mkoa wa Tabora.

Akitoa taarifa ya utekelezaji wa moja ya miradi hiyo – ujenzi wa kiwanda kidogo cha kuchakata mazao ya nyuki katika kijiji cha Nkiniziwa, wilayani Nzega – Kamanda wa Kanda Msaidizi Maendeleo ya Ufugaji Nyuki, Ndg. Nuru Tengeza, amesema mradi huo unalenga kuongeza thamani ya mazao ya nyuki kwa kuwawezesha wafugaji kupata bidhaa bora zilizochakatwa.

“Kiwanda hiki pia kitakuwa kituo cha kutoa mafunzo kwa jamii na wadau wa sekta ya nyuki, kikishirikiana na Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania. Tumeandaa mpango wa kuanzisha shamba darasa katika eneo la msitu jirani,” alisema Tengeza.

Kiwanda hicho kimejengwa kwa ufadhili wa shilingi milioni 111.3 kutoka Mfuko wa Misitu Tanzania na tayari ujenzi wake umekamilika.

Wajumbe wa bodi pia walitembelea mradi wa ujenzi wa jengo la mihadhara katika Chuo cha Mafunzo ya Ufugaji Nyuki Tabora, mradi unaogharimu shilingi milioni 592.1 – ambapo shilingi milioni 500 zimetolewa na Mfuko wa Misitu Tanzania. Hadi sasa, ujenzi huo umefikia asilimia 55.

Mkuu wa Chuo hicho, Ndg. Seme Daudi, amesema kukamilika kwa jengo hilo kutaboresha mazingira ya kujifunzia na kuongeza udahili wa wanafunzi watakaoendeleza sekta ya nyuki kitaalamu.

Ziara hiyo ilihitimishwa kwa kutembelea eneo la mradi wa ujenzi wa Kituo cha Utafiti wa Misitu (TAFORI) Kanda ya Magharibi, katika kijiji cha Kipalapala,nje kidogo ya  mji wa Tabora. Bodi imeeleza kuridhishwa na hatua za awali za maandalizi ya eneo hilo lenye ukubwa wa ekari 10.

Kaimu Meneja wa kituo hicho, James Lyamuya, pamoja na viongozi wengine wa miradi, wamepokea maelekezo ya msingi kutoka kwa bodi na kuahidi kuyatekeleza kikamilifu kwa kuzingatia sheria za ununuzi wa umma na kuhakikisha miradi inakamilika kwa ubora na kwa wakati.

Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 18, 2023
  • SIKU YA KIMATAIFA YA WANAWAKE MACHI 8 March 07, 2024
  • BEI ELEKEZI YA MBOLEA YA CAN KWA KAMPUNI YA YARA June 15, 2022
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MITAALA YA ELIMU TANZANIA BARA March 23, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • BODI YA WADHAMINI MFUKO WA MISITU TANZANIA YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO TABORA.

    May 07, 2025
  • NAIBU WAZIRI MKUU AONGOZA HAFLA YA UWEKAJI WA JIWE LA MSINGI UJENZI WA KIWANDA CHA NGUZO ZA ZEGE TABORA.

    May 03, 2025
  • DKT. BITEKO AIPONGEZA TANESCO NA ETDCO KWA JUHUDI ZA KUBORESHA HUDUMA YA UMEME URAMBO

    May 02, 2025
  • SERIKALI IPO KAZINI KUBORESHA HAKI NA MASLAHI YA WAFANYAKAZI, WAFANYAKAZI NI UTI WA MGONGO WA TAIFA – MHE. SAUDA MTONDOO,

    May 01, 2025
  • Angalia zote

Video

VIJANA WAKAA MEZA MOJA NA RC MKOA WA TABORA
video nyingine

Viungio vya Haraka

  • Maelezo na fomu ya ahadi ya uadilifu kwa watumishi wa umma
  • Guidelines for the use of ICT in government
  • Agriculture
  • MALALAMIKO,PONGEZI NA MAONI INGIA HAPA
  • Bofya hapa Eoffice

Tovuti Muhimu

  • Ikulu
  • Ofisi ya Rais-Tamisemi
  • Ofisi ya Rais-Utumishi
  • SALARYSLIP
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tabora

    S.L.P: 25 Tabora

    Simu: 026 2604058

    Mobile:

    Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa mara
    • Service
    • owner

Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa