• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Nukushi ya malalamiko |
TABORA REGION ADMINISTRATIVE SECRETARY

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi Ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tabora

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Biashara
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo Cha Mawasiliano
      • Community development
    • Muundo
  • Wilaya
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Wilaya ya Urambo
    • Wilaya ya Igunga
    • Wilaya ya Uyui
    • Wilaya ya Kaliua
    • Wilaya ya Sikonge
    • Wilaya ya Nzega
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Tabora
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Halmashauri ya Wilaya ya Igunga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua
    • Halmashauri ya Wilaya Urambo
    • Halmashauri ya Mji wa Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya Sikonge
  • Fursa za Uwekezaji
    • Miombo Project
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi inayoendelea
    • Kilimo
      • Miombo Project
        • Miradi iliyokamilika
        • Miradi inayoendelea
    • Mifugo
    • Opportunity services
    • Viwanda na Biashara
      • New menu item
    • Madini
    • Uvuvi
    • EQUIP-TANZANIA
    • FURSA ZA UWEKEZAJI
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Tafiti
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

MKOA WA TABORA WAPATA ALAMA YA KIJANI KATIKA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE.

Posted on: August 27th, 2025


Na. Mwandishi Wetu, Tabora.

Mkuu wa Wilaya ya Kaliua, Mhe. Dkt. Gelard Mongella, kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Mhe. Paulo Chacha, ameongoza kikao cha tathmini ya mkataba wa lishe, usafi wa mazingira pamoja na malezi na makuzi ngazi ya mkoa, kilichofanyika katika ukumbi mdogo wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tabora.

Akifungua kikao hicho, Katibu Tawala wa Mkoa wa Tabora, Ndg. John Mboya, aliwapongeza wadau wa sekta ya afya, elimu na maendeleo ya jamii kwa ushirikiano wao uliowezesha mkoa kupata alama ya kijani katika utekelezaji wa afua za lishe.

“Kwa hiyo niwapongeze sana kwa kazi nzuri mlioifanya… sasa tunaona green! Hii green ni jambo la kujivunia, hongereni sana,” alisema Dkt.Mboya.

Akizungumza na washiriki wa kikao hicho, Mhe. Dkt. Mongella aliwapongeza wataalamu na viongozi wa halmashauri kwa kazi kubwa waliyoifanya, huku akisisitiza haja ya kuongeza nguvu ili mkoa uendelee kubaki katika daraja la kijani.

“Kwa bidii tuliyoifanya na malengo tuliyowekeana, tuhakikishe tunapanda juu zaidi. Tutumie takwimu tulizonazo kuziba mapungufu yaliyopo ili Tabora iwe kinara katika masuala ya lishe, uchumi na ustawi wa wananchi wake,” alisisitiza Mhe. Mongella

Katika mjadala wa kikao hicho, Katibu Tawala Msaidizi anayeshughulikia Afya mkoani Tabora, Dkt. Honoratha Rutatanisibwa, alieleza kuwa changamoto ya kupasuka kizazi kwa akina mama wajawazito inachangiwa na ukosefu wa elimu ya afya ya uzazi, matumizi ya dawa za asili kwa ajili ya kuongeza uchungu, ushiriki mdogo wa wenza katika kipindi cha ujauzito hadi kujifungua, na kushindwa kuhudhuria kliniki mapema ili kubaini viashiria vya hatari vya uzazi pingamizi.

Dkt. Rutatanisibwa alitoa rai kwa jamii, hususan wanaume, kuwa karibu na wake zao kipindi chote cha ujauzito hadi kujifungua, akisema hatua hiyo itasaidia kupunguza vifo vya mama na mtoto.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Wakurugenzi wa Halmashauri mkoani Tabora, Dkt. John Pima, alihimiza wadau na jamii kuendelea kuelimisha wananchi kuhusu afya ya uzazi ili kuokoa maisha.

Kikao hicho kilihitimishwa kwa utoaji wa vyeti vya pongezi kwa shule na hospitali zilizofanya vizuri katika kuhamasisha lishe bora kupitia bustani za mbogamboga na matunda. Halmashauri za Uyui, Kaliua na Igunga zilitajwa kuwa mfano bora kwa utekelezaji huo.

Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 18, 2023
  • SIKU YA KIMATAIFA YA WANAWAKE MACHI 8 March 07, 2024
  • BEI ELEKEZI YA MBOLEA YA CAN KWA KAMPUNI YA YARA June 15, 2022
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MITAALA YA ELIMU TANZANIA BARA March 23, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • MKOA WA TABORA WAPATA ALAMA YA KIJANI KATIKA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE.

    August 27, 2025
  • RC TABORA AKAMILISHA AHADI MILIONI 15 KWA BONDIA ZUGO, PAMBANO KALI KATI YA ZUGO NA KUMAR KUFANYIKA KESHO TABORA HOTEL

    August 22, 2025
  • “KANISA LIPO TAYARI KUSHIRIKIANA NA SERIKALI KUENDELEZA MAENDELEO TABORA: KARDINALI RUGAMBWA”.

    August 11, 2025
  • TFS YAENDESHA MAFUNZO YA UHIFADHI WA MAZINGIRA DHIDI YA UHARIBIFU WA ARDHI NA MISITU MKOANI TABORA

    August 11, 2025
  • Angalia zote

Video

VIJANA WAKAA MEZA MOJA NA RC MKOA WA TABORA
video nyingine

Viungio vya Haraka

  • Maelezo na fomu ya ahadi ya uadilifu kwa watumishi wa umma
  • Guidelines for the use of ICT in government
  • Agriculture
  • MALALAMIKO,PONGEZI NA MAONI INGIA HAPA
  • Bofya hapa Eoffice
  • Migration Tanzania

Tovuti Muhimu

  • Ikulu
  • Ofisi ya Rais-Tamisemi
  • Ofisi ya Rais-Utumishi
  • SALARYSLIP
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tabora

    S.L.P: 25 Tabora

    Simu: 026 2604058

    Mobile:

    Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa mara
    • Service
    • owner

Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa