• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Nukushi ya malalamiko |
TABORA REGION ADMINISTRATIVE SECRETARY

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi Ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tabora

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Biashara
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo Cha Mawasiliano
    • Muundo
  • Wilaya
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Wilaya ya Urambo
    • Wilaya ya Igunga
    • Wilaya ya Uyui
    • Wilaya ya Kaliua
    • Wilaya ya Sikonge
    • Wilaya ya Nzega
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Tabora
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Halmashauri ya Wilaya ya Igunga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua
    • Halmashauri ya Wilaya Urambo
    • Halmashauri ya Mji wa Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya Sikonge
  • Fursa za Uwekezaji
    • Miombo Project
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi inayoendelea
    • Kilimo
      • Miombo Project
        • Miradi iliyokamilika
        • Miradi inayoendelea
    • Mifugo
    • Opportunity services
    • Viwanda na Biashara
      • New menu item
    • Madini
    • Uvuvi
    • EQUIP-TANZANIA
    • FURSA ZA UWEKEZAJI
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Tafiti
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

TFS YAENDESHA MAFUNZO YA UHIFADHI WA MAZINGIRA DHIDI YA UHARIBIFU WA ARDHI NA MISITU MKOANI TABORA

Posted on: August 11th, 2025


Wakala wa Misitu Tanzania (TFS), kwa kushirikiana na wadau wa mazingira nchini, wameandaa mafunzo maalum kuhusu Mbinu Jumuishi ya Tathmini ya Mazingira na Udhibiti wa Uharibifu wa Ardhi pamoja na kupotea kwa bioanuwai katika misitu ya miombo iliyo kusini magharibi mwa Tanzania. Mafunzo hayo yamefanyika katika ukumbi wa mikutano wa Hoteli ya JB, mjini Tabora.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo, mgeni rasmi Dkt. Deogratias Paul Nyangu alisema kuwa mafunzo hayo ni ya muhimu kwa kuwa Tanzania ni mwanachama wa mkataba wa kimataifa wa kupambana na hali ya jangwa. Alisisitiza kuwa ni wajibu wa wadau wa mazingira kujifunza na kuwa tayari kuchukua hatua madhubuti kushiriki kikamilifu katika vita dhidi ya uharibifu wa ardhi katika maeneo yao.

Mafunzo haya ni sehemu ya utekelezaji wa Mradi wa Usimamizi Shirikishi wa Misitu ya Miombo katika mikoa ya Tabora na Katavi. Mradi huu ulianza Januari 2023 na unatarajiwa kukamilika ifikapo Desemba 2027. Jumla ya washiriki 60 wamehudhuria mafunzo hayo, wakitoka katika halmashauri nne: Mlele, Sikonge, Urambo na Kaliua.

Washiriki wa warsha hiyo ni pamoja na maafisa waandamizi kutoka TFS, wahadhiri wa vyuo vikuu na wawakilishi kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais. Lengo la mafunzo hayo ni kuwajengea uwezo washiriki kutambua hali halisi ya maeneo yaliyoathirika na uharibifu wa ardhi na misitu, pamoja na kuandaa mikakati madhubuti ya kupunguza au kuondoa kabisa changamoto hiyo.

Mafunzo hayo pia yanatumia mbinu za kisasa katika uchambuzi wa taarifa, zikiwemo teknolojia ya mifumo ya taarifa za kijiografia (GIS), ili kubaini maeneo hatarishi na kupanga mipango ya kurekebisha hali ya mazingira.

Mradi huu muhimu unafadhiliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Chakula na Kilimo (FAO), Mfuko wa Mazingira wa Dunia (GEF) pamoja na Wakala wa Misitu Tanzania (TFS).

Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 18, 2023
  • SIKU YA KIMATAIFA YA WANAWAKE MACHI 8 March 07, 2024
  • BEI ELEKEZI YA MBOLEA YA CAN KWA KAMPUNI YA YARA June 15, 2022
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MITAALA YA ELIMU TANZANIA BARA March 23, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • “KANISA LIPO TAYARI KUSHIRIKIANA NA SERIKALI KUENDELEZA MAENDELEO TABORA: KARDINALI RUGAMBWA”.

    August 11, 2025
  • TFS YAENDESHA MAFUNZO YA UHIFADHI WA MAZINGIRA DHIDI YA UHARIBIFU WA ARDHI NA MISITU MKOANI TABORA

    August 11, 2025
  • MAONESHO YA NANENANE KANDA YA MAGHARIBI YAFIKIA TAMATI: BALOZI SIRRO AHAMASISHA WAKULIMA KUONGEZA THAMANI YA MAZAO YAO KWA KUTUMIA VIFUGASHIO BORA.

    August 08, 2025
  • KAMPENI YA KISOMO CHA ELIMU YA WATU WAZIMA YAANZA KWA NGUVU MPYA TABORA

    August 06, 2025
  • Angalia zote

Video

VIJANA WAKAA MEZA MOJA NA RC MKOA WA TABORA
video nyingine

Viungio vya Haraka

  • Maelezo na fomu ya ahadi ya uadilifu kwa watumishi wa umma
  • Guidelines for the use of ICT in government
  • Agriculture
  • MALALAMIKO,PONGEZI NA MAONI INGIA HAPA
  • Bofya hapa Eoffice

Tovuti Muhimu

  • Ikulu
  • Ofisi ya Rais-Tamisemi
  • Ofisi ya Rais-Utumishi
  • SALARYSLIP
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tabora

    S.L.P: 25 Tabora

    Simu: 026 2604058

    Mobile:

    Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa mara
    • Service
    • owner

Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa