• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Nukushi ya malalamiko |
TABORA REGION ADMINISTRATIVE SECRETARY

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi Ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tabora

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Biashara
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo Cha Mawasiliano
    • Muundo
  • Wilaya
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Wilaya ya Urambo
    • Wilaya ya Igunga
    • Wilaya ya Uyui
    • Wilaya ya Kaliua
    • Wilaya ya Sikonge
    • Wilaya ya Nzega
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Tabora
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Halmashauri ya Wilaya ya Igunga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua
    • Halmashauri ya Wilaya Urambo
    • Halmashauri ya Mji wa Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya Sikonge
  • Fursa za Uwekezaji
    • Miombo Project
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi inayoendelea
    • Kilimo
      • Miombo Project
        • Miradi iliyokamilika
        • Miradi inayoendelea
    • Mifugo
    • Opportunity services
    • Viwanda na Biashara
      • New menu item
    • Madini
    • Uvuvi
    • EQUIP-TANZANIA
    • FURSA ZA UWEKEZAJI
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Tafiti
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

KAMPENI YA KISOMO CHA ELIMU YA WATU WAZIMA YAANZA KWA NGUVU MPYA TABORA

Posted on: August 6th, 2025

KAMPENI YA KISOMO CHA ELIMU YA WATU WAZIMA YAANZA KWA NGUVU MPYA TABORA.

Katika hali ya kuamsha ari ya elimu kwa watu wazima nchini, Kampeni ya Uanzishaji na Uimarishaji wa Madarasa ya Kisomo imezinduliwa rasmi mkoani Tabora, ikiwa ni hatua mahsusi ya kitaifa inayolenga kuhakikisha kila Mtanzania anapata fursa ya pili ya kujifunza. Uzinduzi huu umeongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Urambo, Mhe. Khamis Mkanachi, kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Mhe. Paul Chacha, ambapo pamoja na viongozi wengine na wananchi, walijumuika kuonesha mshikamano wa kweli katika kutokomeza ujinga na kuongeza ujuzi miongoni mwa watu wazima.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mhe. Mkanachi alisisitiza kuwa elimu ya watu wazima si hiari tena bali ni hitaji la msingi kwa maendeleo ya taifa. Alieleza kuwa takwimu za asilimia 32 ya watu wasiojua kusoma, kuandika na kuhesabu mkoani Tabora ni changamoto kubwa inayohitaji hatua za dharura. Alieleza kuwa Serikali kupitia Dira ya Maendeleo ya 2050 na mwelekeo wa Ajenda ya Afrika 2063, imeweka mkazo mkubwa katika kujenga jamii yenye maarifa, ujuzi na usawa wa kijinsia, na kwamba elimu jumuishi kwa watu wote ni nyenzo muhimu ya kufanikisha ajenda hizo.

Naye Mkuu wa Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima nchini (TEWW), Prof. Philipo  Sanga, aliweka bayana kuwa taasisi yake imekuwa kinara katika utekelezaji wa mikakati ya kitaifa kupitia programu kama MUKEJA na mbinu ya RIFLEKTI inayowalenga watu wazima katika kupata stadi si tu za KKK, bali pia ujuzi wa maisha, ujasiriamali na utatuzi wa changamoto za kijamii. Alisema kuwa TEWW imeendelea kutoa mafunzo kwa wakufunzi na wawezeshaji kote nchini ili kuongeza ufanisi wa programu hizi, huku lengo kuu likiwa ni kuhakikisha hakuna Mtanzania anayebaki nyuma kielimu.

Aidha, Mhe. Mkanachi alieleza kuwa Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imeendelea kuwekeza kwa kiwango kikubwa katika elimu, ikiwemo elimu nje ya mfumo rasmi. Alitaja Waraka wa Elimu Na. 2 wa mwaka 2021 kuwa mfano wa jitihada hizo, ambapo mabinti waliokatisha masomo wanapewa fursa ya kurejea na kujiendeleza. Alitoa rai kwa halmashauri, taasisi, mashirika binafsi na wadau wa maendeleo kushiriki kwa hali na mali katika kuanzisha na kuimarisha madarasa ya kisomo.

Kwa upande wake, Prof. Sanga alisisitiza kuwa pamoja na mafanikio yaliyopo, bado kuna haja ya kuongeza juhudi zaidi hususani katika maeneo ya vijijini na pembezoni mwa jamii ambako uhitaji wa elimu ni mkubwa. Aliongeza kuwa kampeni hii ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 50 ya TEWW, na inalenga kuwasha tena taa ya matumaini kwa maelfu ya Watanzania waliokata tamaa ya kujifunza. Kauli mbiu ya “Elimu Haina Mwisho” imepewa uhai upya kupitia kampeni hii.

Mwisho, kwa niaba ya Mkoa wa Tabora, Mhe. Mkanachi aliahidi kuwa serikali ya mkoa itaendelea kushirikiana kwa karibu na TEWW katika kuhakikisha ajenda hii muhimu ya elimu ya watu wazima inatekelezwa kikamilifu. Alisisitiza kuwa maendeleo ya kweli hayawezi kupatikana bila elimu, na hivyo kila mmoja anapaswa kuwa balozi wa kusambaza hamasa ya kisomo katika jamii. Katika kutamatisha hafla hiyo, alitangaza rasmi kuzinduliwa kwa kampeni ya kuanzisha na kuimarisha madarasa ya kisomo nchini kote.

Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 18, 2023
  • SIKU YA KIMATAIFA YA WANAWAKE MACHI 8 March 07, 2024
  • BEI ELEKEZI YA MBOLEA YA CAN KWA KAMPUNI YA YARA June 15, 2022
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MITAALA YA ELIMU TANZANIA BARA March 23, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • “KANISA LIPO TAYARI KUSHIRIKIANA NA SERIKALI KUENDELEZA MAENDELEO TABORA: KARDINALI RUGAMBWA”.

    August 11, 2025
  • TFS YAENDESHA MAFUNZO YA UHIFADHI WA MAZINGIRA DHIDI YA UHARIBIFU WA ARDHI NA MISITU MKOANI TABORA

    August 11, 2025
  • MAONESHO YA NANENANE KANDA YA MAGHARIBI YAFIKIA TAMATI: BALOZI SIRRO AHAMASISHA WAKULIMA KUONGEZA THAMANI YA MAZAO YAO KWA KUTUMIA VIFUGASHIO BORA.

    August 08, 2025
  • KAMPENI YA KISOMO CHA ELIMU YA WATU WAZIMA YAANZA KWA NGUVU MPYA TABORA

    August 06, 2025
  • Angalia zote

Video

VIJANA WAKAA MEZA MOJA NA RC MKOA WA TABORA
video nyingine

Viungio vya Haraka

  • Maelezo na fomu ya ahadi ya uadilifu kwa watumishi wa umma
  • Guidelines for the use of ICT in government
  • Agriculture
  • MALALAMIKO,PONGEZI NA MAONI INGIA HAPA
  • Bofya hapa Eoffice

Tovuti Muhimu

  • Ikulu
  • Ofisi ya Rais-Tamisemi
  • Ofisi ya Rais-Utumishi
  • SALARYSLIP
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tabora

    S.L.P: 25 Tabora

    Simu: 026 2604058

    Mobile:

    Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa mara
    • Service
    • owner

Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa