• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Nukushi ya malalamiko |
TABORA REGION ADMINISTRATIVE SECRETARY

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi Ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tabora

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
  • Utawala
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Biashara
    • Idara
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo Cha Mawasiliano
    • Muundo
  • Wilaya
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Wilaya ya Urambo
    • Wilaya ya Igunga
    • Wilaya ya Uyui
    • Wilaya ya Kaliua
    • Wilaya ya Sikonge
    • Wilaya ya Nzega
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Tabora
    • Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
    • Halmashauri ya Wilaya ya Igunga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua
    • Halmashauri ya Wilaya Urambo
    • Halmashauri ya Mji wa Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nzega
    • Halmashauri ya Wilaya Sikonge
  • Fursa za Uwekezaji
    • Miombo Project
      • Miradi iliyokamilika
      • Miradi inayoendelea
    • Kilimo
      • Miombo Project
        • Miradi iliyokamilika
        • Miradi inayoendelea
    • Mifugo
    • Opportunity services
    • Viwanda na Biashara
      • New menu item
    • Madini
    • Uvuvi
    • EQUIP-TANZANIA
    • FURSA ZA UWEKEZAJI
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Tafiti
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

MAONESHO YA NANENANE KANDA YA MAGHARIBI YAFIKIA TAMATI: BALOZI SIRRO AHAMASISHA WAKULIMA KUONGEZA THAMANI YA MAZAO YAO KWA KUTUMIA VIFUGASHIO BORA.

Posted on: August 8th, 2025


Mkuu wa mkoa wa Kigoma IGP (Mstaafu) Balozi Simon Nyakoro Sirro, amehitimisha rasmi maonesho ya sikukuu ya wakulima nane nane yaliyofanyika kikanda mkoani Tabora katika viwanja vya Fatma Mwasa,Ipuli – Manispaa ya Tabora. . Katika hotuba yake, Balozi Sirro alitoa shukrani kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa uwekezaji mkubwa katika sekta za kilimo, mifugo na uvuvi, pamoja na wadau wote walioshiriki kufanikisha maonesho haya.

Akizungumzia kaulimbiu ya mwaka huu “Chagua Viongozi Bora kwa Maendeleo Endelevu ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi 2025”, Balozi Sirro aliwahimiza wananchi wa Tabora na Kigoma kujitokeza kwa wingi katika uchaguzi ujao, wakichagua viongozi watakaosimamia maendeleo ya sekta hizo. Alisisitiza umuhimu wa kutumia elimu, teknolojia na ubunifu uliopatikana kupitia maonesho haya ili kuongeza tija na thamani katika uzalishaji.

Kwa upande wa kilimo, alieleza hatua za Serikali katika kutoa mbolea na mbegu bora kwa ruzuku, kuhakikisha upatikanaji wa pembejeo kwa wakati, na kuimarisha taasisi za utafiti kama TARI na SUA. Aidha, aliwasihi wakulima kujiandikisha ili kuendelea kunufaika na mpango wa ruzuku na kutumia mbegu zenye ubora unaodhibitiwa na mamlaka husika.

Katika sekta ya mifugo, alibainisha kampeni kubwa ya chanjo iliyoanzishwa na Rais Samia, ikilenga kupunguza vifo na magonjwa ya mifugo. Wafugaji walihimizwa kuchangamkia huduma za taasisi za serikali ikiwemo TVLA na ZVC, ili kupata huduma za chanjo, uchunguzi wa magonjwa, vibali na mafunzo ya ufugaji bora. Sekta ya uvuvi na ufugaji nyuki pia zilitajwa kama maeneo yenye fursa kubwa, zikichochewa na uwepo wa vituo maalum vya mafunzo na uzalishaji katika kanda.

Balozi Sirro pia amesisitiza kuboresha namna wakulima wanavyofungasha bidhaa zao kwa kutumia vifungashio bora lakini vilivyobeba thamani ya bidhaa yenyewe, ikiwemo kuonesha aina ya virutubisho au madini yaliyomo. Amewashauri wakulima kushirikiana na Shirika la Viwango Tanzania (TBS) ili kuhakikisha bidhaa wanazozalisha zinakidhi viwango na ubora unaokubalika kitaifa na kimataifa, hatua itakayoongeza ushindani kwenye masoko ya ndani na nje ya nchi.

Akihitimisha, alisisitiza umuhimu wa kuongeza thamani ya mazao, kuimarisha mabanda ya kudumu, na kuandaa mikakati ya matumizi endelevu ya viwanja vya maonesho mwaka mzima. Aliwataka makampuni ya mawasiliano na taasisi za kifedha kushirikiana katika kudhamini maonesho haya ili kuongeza ushiriki na kutoa elimu kwa wakulima, wafugaji na wavuvi. “Maadhimisho haya ya Nanenane Kanda ya Magharibi kwa mwaka 2025 yamefikia kilele chake leo,” alitangaza huku akipokea shangwe za washiriki na wananchi.

Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 18, 2023
  • SIKU YA KIMATAIFA YA WANAWAKE MACHI 8 March 07, 2024
  • BEI ELEKEZI YA MBOLEA YA CAN KWA KAMPUNI YA YARA June 15, 2022
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MITAALA YA ELIMU TANZANIA BARA March 23, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • “KANISA LIPO TAYARI KUSHIRIKIANA NA SERIKALI KUENDELEZA MAENDELEO TABORA: KARDINALI RUGAMBWA”.

    August 11, 2025
  • TFS YAENDESHA MAFUNZO YA UHIFADHI WA MAZINGIRA DHIDI YA UHARIBIFU WA ARDHI NA MISITU MKOANI TABORA

    August 11, 2025
  • MAONESHO YA NANENANE KANDA YA MAGHARIBI YAFIKIA TAMATI: BALOZI SIRRO AHAMASISHA WAKULIMA KUONGEZA THAMANI YA MAZAO YAO KWA KUTUMIA VIFUGASHIO BORA.

    August 08, 2025
  • KAMPENI YA KISOMO CHA ELIMU YA WATU WAZIMA YAANZA KWA NGUVU MPYA TABORA

    August 06, 2025
  • Angalia zote

Video

VIJANA WAKAA MEZA MOJA NA RC MKOA WA TABORA
video nyingine

Viungio vya Haraka

  • Maelezo na fomu ya ahadi ya uadilifu kwa watumishi wa umma
  • Guidelines for the use of ICT in government
  • Agriculture
  • MALALAMIKO,PONGEZI NA MAONI INGIA HAPA
  • Bofya hapa Eoffice

Tovuti Muhimu

  • Ikulu
  • Ofisi ya Rais-Tamisemi
  • Ofisi ya Rais-Utumishi
  • SALARYSLIP
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tabora

    S.L.P: 25 Tabora

    Simu: 026 2604058

    Mobile:

    Barua Pepe: ras.tabora@tamisemi.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa mara
    • Service
    • owner

Haki Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora .Haki zote zimehifadhiwa